Ticker

6/recent/ticker-posts

AUDIO:YANGA WATANGAZA AGENDA ZA MKUTANO WAO MKUU,ziko hapa

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.AUG 5,2016 SAA 12:53 JIONI

Hatimae uongozi wa klabu ya Young Africans, umetangaza ajenda za mkutano mkuu wa wanachama uliopangwa kufanyika kesho katika
ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

Young Africans ilitoa taarifa ya kuitishwa kwa mkutano huo mkuu mwanzoni mwa juma hili pasina kuwa na agenda ambazo zitajadiliwa halia mbayo ilizua tafrani miongoni mwa wanachama na kufikia hatua kwa baadhi yao kuuita mkutano huo ni batili.

Meneja wa masoko na uratibu wa matawi na wanachama wa Young Africans, Omar Kaya alibeba jukumu la kuzitaja agenda za mkutano mkuu wa wanachama ambao umepangwa kuanza mishale ya saa tatu asubuhi.


Hata hivyo suala la kubadilishwa kwa mfumo uendeshwaji nalo limezungumza na Meneja wa masoko na uratibu wa matawi na wanachama wa Young Africans, Omar Kaya baada ya kuibuka kwa tetesi kutoka kwa baadhi ya wanachama ambao walionyesha kupotezwa na maazimio yaliyofikiwa na wapinzani wao Wekundu wa msimbazi Simba mwishoni mwa juma lililopita.

SIKILIZA HAPA

Wakati huo huo Young Africans wameohoji zoezi la kukabidhi vifaa ambalo lilifanywa jana na wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, kampuni ya mawasilino ya Vodacom kufuatia nembo ya kampuni ya vifaa hivyo kutokua na maslahi na klabu yao pamoja na klabu nyingine zitakazoshiriki ligi hiyo.

Omar Kaya amesema kuna haja kwa TFF kupitia bodi ya ligi wakalitolea ufafanuzi suala hilo ambalo linaonekana kumnufaisha zaidi mdhamini wa ligi kuu pamoja na kampuni inayoonekana katika vifaa vilivyotolewa hapo jana

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)


Post a Comment

0 Comments