Ticker

6/recent/ticker-posts

AUDIO/PICHA:NI MANJI MWANZO MWISHO,APEWA TIMU KWA MIAKA 10,MKEMI,NYEZI NA REFA WA SIMBA 5 - 0 YANGA WATIMULIWA

 Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.AUG 6,2016 SAA 01:30 USIKU
Mwenyekiti wa Yanga Yusuf Manji akizungumza hii leo

Historia imeandikwa kwa klabu ya Yanga siku ya Leo 6 Aug.2016 katika Mkutano Mkuu wa dharula uliofanyika leo ukumbi wa
Diamond jubilee, Dar es Salaam baada ya Wanachama hiyo ambayo ni mabingwa wa Tanzania bara kukubali kumkodisha klabu hiyo Mwenyekiti wao, Yusuf Manji kwa miaka 10 .


Katika mkutano huo Manji ameomba apewe klabu hiyo kwa miaka 10 na katika kipindi hicho atakuwa anachukua asilimia 75 ya mapato ya timu, huku asilimia 25 ikibaki kwa wanachama.
Wanachama wa Yanga wakifuatilia Mkutano

mkutano huo umekubali kipindi hicho cha miaka 10, timu, nembo ya klabu zote zitakuwa chini ya Manji.

Katika hatua nyingine mkutano huo umeazimia kuwafukuza uanachama, wanachama watatu wa klabu hiyo, Ayoub Nyenzi, Salum Mkemi na Hashim Abdallah walifukuzwa.
Hashim Abdallah alikuwa ni mjumbe wa kamati ya utendaji wa Yanga,lakini pia ni Mwamuzi aliyechezesha mchezo  wa SIMBA 5 - 0 YANGA  , pichani ni Hashim Abdallah, akimpa kadi ya njano aliyekuwa golikipa wa timu ya Yanga, Said Kasalama katika mchezo huo baada ya kumdondosha Emmanuel Okwi alipokuwa ndani ya eneo la penalti na kisha kupigiwa adhabu hiyo, iliyopigwa na marehemu Patrick Mafisango na kufanya Simba hadi wakati huo kuongoza kwa mabao 3-0.PICHA NA:wwwbayanablogspotcom.blogspot.com
Taarifa za mapungufu ya wajumbe wa kamati ya utendaji pamoja na wanachama hao wa Young Africans ziliwasilishwa  katika mkutano huo na kaimu mtendaji mkuu Baraka Deusdetit.
Kaimu mtendaji mkuu Baraka Deusdetit

SIKILIZA HAPA


Mara baada ya kutolewa kwa taarifa hiyo Manji aliwaambia wanachama hayuko tayari kufanya kazi na Wajumbe hao wa Kamati ya Utendaji na akaomba wanachama wanaowataka wajitokeze kupiga kura, lakini hakuna aliyeinuka.

Baada ya kurudia kuita mara tatu, Hashim pekee kati ya watatu hao ambaye alikuwepo mkutanoni ukumbi wa Diamond Jubilee, akainuka na kuondoka.
Mwanachama mwingine, Siza Lyimo ambaye Manji alitaka aondoke, yeye aliomba msamaha na wanachama wakamsamehe na Mwenyekiti huyo akabariki msamaha huo.

Mkemi na Nyenzi hawakutokea kwenye Mkutano huo.

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

Post a Comment

0 Comments