Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.AUG 17,2016 SAA 06:34 MCHANA
Katika mchezo wa
Ngao ya Jamii hii Leo unaoshiria kufunguliwa kwa pazia la msimu mpya wa Ligi Kuu
ya Vodacom Tanzania Bara
(VPL) 2016/17,kutakutanisha wababe wawili ambao ni Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati Azam FC,mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga Sc na mchezo huo utapigwa hii leo saa 10.30 jioni.
(VPL) 2016/17,kutakutanisha wababe wawili ambao ni Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati Azam FC,mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga Sc na mchezo huo utapigwa hii leo saa 10.30 jioni.
Azam FC inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na makocha wapya kutoka
Hispania, wakiongozwa na Kocha Mkuu Zeben Hernandez.
Ukiachilia mbali ujio wa makocha wapya, pia kuna baadhi ya sura kwa
upande wa wachezaji, Azam FC ikiwasajili Wazimbabwe Bruce Kangwa,
Francisco Zekumbawire, Muivory Coast Gonazo Bi Thomas, Waghana Enock
Atta Agyei na beki kisiki Daniel Amoah.
Rekodi/Takwimu
Hii ni mara ya nne timu hizo kukutana kwa mwaka huu, ambapo Januari
walikutana kwenye mchezo wa Kombe la Mapinduzi na kuisha kwa sare ya bao
1-1, mtanange huo ulifuatiwa na ule wa mzunguko wa wa pili wa ligi
ambao uliisha kwa sare nyingine ya 2-2 kabla ya Yanga kushinda 3-1
katika fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup).
Katika hatua nyingine, hii ni mara ya nne mfululizo kwa timu hizo
kukutana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii, Yanga ikifanikiwa kuibuka na
ushindi mara zote.
Walianza kukutana mwaka 2013, Yanga wakishinda bao 1-0, lililofungwa
na Salum Telela, ikashinda tena 3-0 (2014) kabla ya mwaka jana kushinda
kwa changamoto ya mikwaju ya penalti 8-7 kufuatia sare ya 0-0 baada ya
dakika 90 za muda wa kawaida kumalizika.

0 Comments