Mabingwa Tanzania bara Dar es salaam Young Africans wanatarajiwa kurejea nchini wakati wowote kuanzia kesho tayari
kwa maandalizi ya mchezo wa pili wa hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika CAF.
Mkuu wa idara ya habari na mawasilino wa klabu hiyo iliyosalia kwenye michuano ya kimataifa katika ukanda wa Afrika mashariki, Jerry Murro amesema kikosi chao kitaweka kambi hapa nchini kutokana na hali ya hewa ya nchini Uturuki kutofautiana na ya hapa nchini ambapo mchezo wa pili dhidi ya TP Mazembe utakapochezwa.
Muro pia amezungumzi mchezo wa jana waliocheza dhidi ya Mo Bejaia na kushuhudia wakibamizwa bao moja kwa sifuri.
SIKILIZA HAPA
Wakati huo huo Muro amerusha dongo kwa wapinzani wao jadi Simba ambao walizuia beki wa pembeni wa Hassn Kessy kutokucheza mchezo wa jana baada ya kuwasilisha barua kwenye makao ya shirikisho la soka barani Afrika CAF, kwa madai ya kuwa na mkataba na mchezaji huyo ambaye alijiunga na Young Africans mwishoni mwa mwezi uliopita.

0 Comments