Jose Mourinho amesaini mkataba wake wa kuwa kocha mpya wa Manchester United.
Tangazo rasmi kutoka klabu linatarajiwa kutoka siku ya Ijumaa.
Mourinho, ambaye amekuwa nje ya kazi tangu alipotimuliwa na Chelsea mwezi Desemba , anachukuwa nafasi mshauri wake wa zamani Van Gaal, ambaye amefukuzwa kazi na United siku mbili baada ya kushinda Kombe la FA dhidi ya Crystal Palace katika uwanja wa Wembley.

0 Comments