Raheem
Sterling anajiandaa kuanza tena mazungumzo ya mkataba wake na Liverpool baadaye
wiki hii, lakini inakusudia huenda
akawaambia kuwa yeye hana mpango wa kusaini mkataba
mpya, kulingana na vyanzo Mbalimbali vya habari.
Winga huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 20 atafanya
uamuzi kuhusu mustakabali wake mwishoni mwa wiki hii, wakati yeye atakapokutana na meneja Brendan Rodgers pamoja na mtendaji mkuu Ian
Ayre.
Na baada ya mkutano huo, itakuwa wazi kama anatarajia kukaa katika uwanja wa Anfield, au kuondoka katika klabu hiyo.
Kama ilivyo sasa, vyanzo vya habari vinatarajia kwamba Sterling atawaambia Liverpool kwamba yeye hataki kusaini mkataba mpya.
Lakini mkataba
wake wa sasa bado una miaka miwili kuisha na mchezaji huyo
mwezi uliopita, alisema kwamba uamuzi wake si kuhusu fedha, lakini atakuwa
na hamasa kwa mapenzi yake kwa kushinda vikombe.
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

0 Comments