Ticker

6/recent/ticker-posts

RAHEEM STERLING HANA MPANGO WA KUSAINI MKATABA MPYA NA LIVERPOOL

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.May .19,2015 SAA 06:54 USIKU
Raheem Sterling: No plans to sign new deal.
Raheem Sterling anajiandaa kuanza tena mazungumzo ya mkataba wake na Liverpool baadaye wiki hii, lakini inakusudia huenda
akawaambia kuwa yeye hana mpango wa kusaini mkataba mpya, kulingana na vyanzo Mbalimbali vya habari.

Winga huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 20  atafanya uamuzi kuhusu mustakabali wake mwishoni mwa wiki hii, wakati yeye atakapokutana na meneja Brendan Rodgers pamoja na mtendaji mkuu Ian Ayre.

Na baada ya mkutano huo, itakuwa wazi kama anatarajia kukaa katika uwanja wa Anfield, au kuondoka katika klabu hiyo.

Kama ilivyo sasa, vyanzo vya habari vinatarajia kwamba Sterling atawaambia Liverpool kwamba yeye hataki kusaini mkataba mpya. 

Lakini mkataba wake wa sasa bado una miaka miwili kuisha na mchezaji huyo mwezi uliopita, alisema kwamba uamuzi wake si kuhusu fedha, lakini atakuwa na  hamasa kwa mapenzi yake kwa kushinda vikombe. 

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)  

Post a Comment

0 Comments