Usiku wa jana kulikuwa na mchezo mmoja wa ligi kuu ya England ambapo klabu ya Manchester City imepokea
kichapo cha mabao 2-1 kutoka katika klabu ya Crystal Palace.
Lakini licha ya kichapo hiko, Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini anasema kuwa yeye alifurahishwa na utendaji kazi wa klabu yake licha ya kufungwa, mabao hayo 2-1 na klabu ya Crystal Palace.
Pellegrini ambaye siku ya jumapili atakuwa na mchezo muhimu wa Manchester derby, atapokwenda Old Trafford kucheza na manchester United,ameomba radhi kwa matokeo ya mchezo huo,lakini amekiri, kupoteza nafasi nyingi za mabao.
"Tulikuwa na nafasi nyingi na tulikosa mabao zaidi,lakini naomba radhi sana kwa jinsi timu yangu ilivyocheza kwa sababu nadhani sisi tucheza vizuri,"
" Si zungumzii juu ya taji, sisi tunataka kushinda michezo yetu tu . Kila wakati (tunashuka) pointi, ni pigo kubwa. Mwishoni mwa msimu, kila hatua ambayo unapoteza ni gharama kubwa".
"Michezo saba ijayo ni muhimu sana - pointi 21, Kwa kawaida mabingwa katika ligi,kuna kuwa na tofauti ya pointi moja au pointi mbili tu (dhidi ya timu ya pili) , hivyo tunapaswa kuendelea kushinda pointi nyingi kama tunaweza".
"Na rudia, sisi tunafikiri juu ya nini tunaweza kufanya tu, na kujaribu kushinda michezo yetu na mwishoni mwa msimu tutaona tulipo katika msimbamo wa ligi."
Mabao ya Crystal Palace kutoka kwa wachezaji wake Glenn Murray kipindi cha kwanza na Jason Puncheon kipindi cha pili,yaliizamisha jahazi la Manchester City,licha ya bao la kufutia machozi kutoka kwa Yaya Toure dakika ya 78.
English Barclays Premier League | LOGS
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | Chelsea | 30 | 21 | 7 | 2 | 63 | 26 | 37 | 70 |
| 2 | Arsenal | 31 | 19 | 6 | 6 | 62 | 32 | 30 | 63 |
| 3 | Manchester United | 31 | 18 | 8 | 5 | 55 | 28 | 27 | 62 |
| 4 | Manchester City | 31 | 18 | 7 | 6 | 63 | 30 | 33 | 61 |
| 5 | Liverpool | 31 | 16 | 6 | 9 | 45 | 36 | 9 | 54 |
| 6 | Tottenham Hotspur | 31 | 16 | 6 | 9 | 50 | 45 | 5 | 54 |
| 7 | Southampton | 31 | 16 | 5 | 10 | 42 | 22 | 20 | 53 |
| 8 | Swansea City | 31 | 13 | 7 | 11 | 37 | 39 | -2 | 46 |
| 9 | West Ham United | 31 | 11 | 9 | 11 | 41 | 39 | 2 | 42 |
| 10 | Stoke City | 31 | 12 | 6 | 13 | 35 | 39 | -4 | 42 |
| 11 | Crystal Palace | 31 | 10 | 9 | 12 | 38 | 42 | -4 | 39 |
| 12 | Everton | 31 | 9 | 10 | 12 | 39 | 42 | -3 | 37 |
| 13 | Newcastle United | 31 | 9 | 8 | 14 | 33 | 49 | -16 | 35 |
| 14 | West Bromwich Albion | 31 | 8 | 9 | 14 | 28 | 43 | -15 | 33 |
| 15 | Sunderland | 31 | 5 | 14 | 12 | 24 | 44 | -20 | 29 |
| 16 | Hull City | 31 | 6 | 10 | 15 | 29 | 43 | -14 | 28 |
| 17 | Aston Villa | 31 | 7 | 7 | 17 | 20 | 42 | -22 | 28 |
| 18 | Burnley | 31 | 5 | 11 | 15 | 26 | 49 | -23 | 26 |
| 19 | Queens Park Rangers | 31 | 7 | 4 | 20 | 35 | 55 | -20 | 25 |
| 20 | Leicester City | 30 | 5 | 7 | 18 | 29 | 49 | -20 | 22 |
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) .
0 Comments