Nahodha wa England Wayne Rooney ana furaha kubwa kwa kuwa atacheza na Harry Kane katika safu ya ushambuliaji katika mchezo wa
kirafiki leo Jumanne dhidi ya Italia.
Roy Hodgson alithibitisha katika mkutano wa kabla ya mechi na vyombo vya habari,kuwa Kane mchezaji wa Tottenham Hotspur,ataanza katika kikosi cha England mjini Turin baada kufunga goli lake la kwanza akiwa chini ya sekunde 79 baada ya kuanzishwa kwake kutoka benchi dhidi ya timu ya Lithuania Ijumaa iliyopita katika dimba la Wembley.
Hodgson hakutaka kutangaza kikosi kizima cha timu yake, lakini alisema alikuwa na furaha kubwa na matarajio ya kuwa, Kane na nahodha Wayne Rooney wataanza katika mchezo huo,utakaopigwa mjini Turin.
"Ni vizuri sana kuwaona wote wawili kwenye uwanja kwa pamoja," . "Wao wamefanya mengi katika mazoezi na mimi niko radhi kuwaona wakicheza pamoja tangu mwanzo. Harry hakika anastahili nafasi yake na mimi nina angalia mbele katika mchezo".
"Tunachukulia kwa umakini sana. Ni fursa kubwa kwa wachezaji ambao walikuwa hawana nafasi katika kufuzu,kuonyesha kweli wanastahili nafasi yao katika kikosi, na kwamba wao wako vizuri vya kutosha kuchukua nafasi ya wachezaji ambao nimekuwa nikiwachagua kabla yao".alisema Hodgson
| Sir Bobby Charlton |
Kwa upande wa Rooney ambaye amebakisha mabao mawili kwa timu ya taifa kufikia rekodi ya Sir Bobby Charlton ya mabao 49, mshambuliaji huyo anasisitiza kuwa,anatumaini Harry Kane ataendelea kuwa katika fomu nzuri kwa timu ya England,na usiku wa leo ni usiku mkubwa kwa mchezaji huyo,kwa kuanza naye mechi yake ya kwanza, na ana uhakika atafanya vizuri.
March 31
02:30
? - ?
04:00
? - ?
12:30
? - ?
13:00
? - ?
13:25
? - ?
14:00
? - ?
14:30
? - ?
16:00
? - ?
16:00
? - ?
18:00
? - ?
19:00
? - ?
19:00
? - ?
19:00
? - ?
20:00
? - ?
20:30
? - ?
21:00
? - ?
21:15
21:30
? - ?
21:30
? - ?
21:30
? - ?
21:45
? - ?
21:45
? - ?
22:45
? - ?
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) .
0 Comments