Ticker

6/recent/ticker-posts

TAARIFA KUHUSU AGUERO KUKOSA MECHI YA MANCHESTER DERDY,PAMOJA NA TETESI ZA UHAMISHO WAKE KWENDA BARCELONA

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA March. 21,2014 SAA 02:22 USIKU

Mfungaji bora  wa Manchester City Sergio Aguero atakosa derby ya wiki ijayo dhidi ya Manchester United kutokana na kuwa
majeruhi, meneja Manuel Pellegrini amethibitisha leo siku ya Ijumaa.

Aguero anaendelea kuuguza majeraha ambayo aliyapata wakati timu yake ikicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa ambao walifungwa na Barcelona wiki iliyopita na Pellegrini anasema kwamba "hakuna nafasi" kwa mchezaji huyo kuanza safari ya Old Trafford siku ya Jumanne. 

Aguero, ambaye alifunga mabao 26 msimu huu, anaweza  kurudi katika mchezo dhidi ya Arsenal siku ya tarehe 29 March.

"Sisi bado hatujui, lakini labda wiki ijayo ataanza kufanya kazi na kikosi," Pellegrini alisema.
 
"Sidhani kama ni wiki nzima. Labda mwishoni mwa wiki anaweza kuwa na kikosi na kuanza mazoezi."

 Alipoulizwa kama nyota huyo wa kimataifa wa Argentina atakuwa katika mpambano watakaokutana na United, Pellegrini alijibu: "Kwa United,hapana,hana nafasi." 

Akizungumza kabla ya timu yake ambayo itakuwa nyumbani ikipambana na Fulham siku ya Jumamosi, Pellegrini pia aliongeza kwa kukanusha uvumi kuwa Aguero yuko katika harakati za uhamisho kwenda Barcelona. 

"Hatuwezi kuzungumza kila wiki kuhusu wachezaji ambao wako hapa Manchester City na wachezaji kuwa wata kwenda nje. Yeye ni mchezaji wa Manchester City, yeye anafuraha sana hapa katika klabu na tuna furaha sana pamoja naye pia." 

Post a Comment

0 Comments