Ticker

6/recent/ticker-posts

ALICHOKISEMA ROBERTO MARTNEZI JUU YA MACHESTER UNITED KUFANYA MAZUNGUMZO NA HUYU MCHEZAJI

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA March. 20,2014 SAA 11:56 JIONI

Meneja wa Everton Roberto Martinez imekataa taarifa kuwa Manchester United iko katika mazungumzo ya  kumasaini mlinzi wa
klabu hiyo, Seamus Coleman.

Mlinzi huyo wa Jamhuri ya Ireland amekuwa akitolewa macho katika msimu huu,kufuatia utendaji wake wa kazi katika kikosi cha  Evarton , na mkataba wake na timu hiyo ya Goodison Park bado unaendelea hadi Juni 2018.

Hata hivyo, Meneja wa United David Moyes ameripotiwa kuwa na nia ya kumleta mchezaji huyo mwenye miaka  25 ndani ya  Old Trafford katika majira ya joto, lakini Mhispania Martinez ameweka  ngumu ya kuhakikisha kuwa hakuna mtu atakayeweza kuwasiliana na kujadili juu ya  mchezaji huyo anayemtegemea katika siku zijazo. 

Alisema: "Ni lazima kuwe na tofauti kwa Seamus Coleman kwa sababu sisi hatujawai kuwa na majadiliano yoyote na mtu yeyote". 

"Nadhani ukweli ni kwamba Seamus amekuwa na msimu mzuri sana na tunataka  kuendelea na tunamatumaini katika kipindi cha michezo 10, anaweza kuendelea na kiwango cha juu kwani ameonyesha na bado anaendelea". alisema Roberto Martinez

Post a Comment

0 Comments