Ticker

6/recent/ticker-posts

TAARIFA YA PETER ODEMWINGIE JUU YA KWENDA BRAZIL

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA March. 20,2014 SAA 11:56 JIONI

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Nigeria, Peter Odemwingie ameelezea wasiwasi wake wa kama ataweza kuwa katika  kikosi
cha Nigeria katika  fainali za Fifa za Kombe la Dunia nchini  Brazil mwaka huu 2014 .

Hii ni kulingana na mchezaji mwenzake katika  Ligi kuu ya Uiingereza katika klabu ya Stoke City, Asmir Begovic.

Begovic ambaye ana kofia 28 kwa timu yake ya taifa Bosnia-Herzegovina anaweza kukutana na Odemwingie wakati wa timu ya Ulaya itakapokutana na Nigeria Super Eagles katika kombe la dunia 2014 Juni 14 katika uwanja Pantanal, Cuiaba.

Odemwingie hakuwa mchezaji katika kikosi cha Nigeria tangu Februari 29, 2012 katika Kombe la mataifa ya Afrika katika mchezo wa  kufuzu  dhidi ya Rwanda  huko Kigali. 

Bergovic sasa amebaini kuwa Odemwingie hajui kama yeye atakuwa pamoja na Stephen Keshi katika kikosi cha kombe la dunia la FIFA 2014.

"Mimi na Peter tumekuwa  na mazoezi kila siku. Yeye  hana uhakika kabisa wa kwenda katika kikosi bado na sisi sote huwa tunaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha tunapata nafasi ya kwenda Brazil". 

 

Post a Comment

0 Comments