Ticker

6/recent/ticker-posts

ALICHOKISEMA PABLO ZABALETA BAADA YA KUTOLEWA KWA KADI NYEKUNDU

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 13,2014 SAA 11:O JIONI

Beki wa Manchester City Pablo Zabaleta amemshutumu mwamuzi wa Kifaransa Stephane Lannoy kwa kumkosoa mwamuzi huyo
kuwa "alifanya maamuzi ya kutisha" kwa Manchester City ambayo walifungwa mabao 2-1 na Barcelona.

Mlinzi huyo wa Argentina,Zabaleta alitolewa nje katika uwanja wa Nou Camp kwa kadi  ya nyekundu baada ya kumzonga mwamuzi Lannoy  kwa sababu ya kushindwa kutoa adhabu wakati Edin Džeko alipoonekana kufanyiwa madhambi na Gerard Pique ndani ya boksi.

Zabaleta mara baada ya kusisitiza kwamba City lazima wapewe Penalti baada ya Džeko kufanyiwa tukio hilo, na anadai kuwa yeye bado yuko katika sintofahamu ya kwa nini alitolewa nje kwa kadi hiyo ya pili ya njano. 
Off you go: Pablo Zabaleta was sent off for a second booking for disputing a penalty appeal with the referee
Nje kabisa: Pablo Zabaleta alitolewa nje kwa kadi ya pili ya njano na  mwamuzi
"ilikuwa ni wazi sana," Zabaleta alisema. "Nadhani Pique alikuwa nyuma yangu na alifanya kukabiliana na Džeko na mwamuzi alikuwa mita mbili tu kutoka umbali". 

"sijui ni kwa nini alinitoa mimi wakati nilikwenda kwake kuzungumza naye kwa njia nzuri". 

"kidogo nilikuwa na hasira kwa sababu yeye hakutoa adhabu, lakini mimi nimekuwa na heshima sana kwake". 

"Nilichanganyikiwa. Nadhani ni uamuzi wa kutisha". 

"Wakati mwingine mchezo unaharibiwa kwa sababu unajaribu kupata matokeo, na wakati mwingine maamuzi ya kutisha yanakuja kwa sababu ya Refa kuwa na hasira kidogo." 

Zabaleta slams referee Lannoy
 

Post a Comment

0 Comments