Ticker

6/recent/ticker-posts

ALICHOKIJIBU RAIS WA INTER MILAN JUU YA FERNANDO TORRES PAMOJA NA JAVIER HERNANDEZ

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 11,2014 SAA 09:50 USIKU
Rais wa Inter Milan Erick Thohir amekanusha kufanya mazungumzo  juu ya uhamisho wa Javier Hernandez au Fernando
Torres.
Hernandez ambaye imekuwa na jukumu dogo katika klabu ya Manchester United msimu huu na amekuwa akihusishwa na taarifa za kuondoka katika klabu hiyo ya Old Trafford.

Inter wametajwa kutoa ofa kwa Mmexico huyo,na kuwa tayari  kupereka ofa nzuri ili kumleta  pamoja na mchezaji mwenzake wa  United Nemanja Vidic msimu ujao, lakini Thohir anasisitiza kuwa hakuna mipango huo wa kufanya uvamizi mara mbili katika klabu ya Manchester. 

Thohir pia alizitupilia mbali ripoti ya kumuunganisha Torres na Inter katika mpango wa muda mrefu wa baadaye, ambapo Chelsea inaendelea kuwa chanzo cha uvumi. 

"Chicharito ni mchezaji mzuri lakini sisi hatukuongea na yeye wala na Torres," Thohir aliwaambia waandishi wa habari, kabla ya kuhojiwa juu ya hatima ya Esteban Cambiasso na Walter Samuel ndani ya klabu hiyo. 

Cambiasso, 33, na Muargentina mwenzake Samuel, 35, ni miongoni mwa wa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu. 

Mkataba wa Rodrigo Palacio umebakisha mwaka kumalizika  lakini mshambuliaji huyo tayari alitangaza kuwa yeye yuko katika mazungumzo kuhusu kutanua mkataba. 

"Na mwisho wa msimu sisi tutathmini wachezaji wote na kuamua ambaye ataishi na ambaye ataondoka," alisema Thohir.
 
"Tuko katika mazungumzo ya kuongeza mkataba na Palacio."
 

Post a Comment

0 Comments