Ticker

6/recent/ticker-posts

LA LIGA:HII NDIO KAULI YA RAIS MPYA WA BARCELONA KUHUSIANA NA MUSTAKABARI WA MESSI

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA JANU. 28,2014 SAA 09:58 ALFAJIRI

Rais mpya wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amesisitiza Lionel Messi hauzwi na anasema klabu hiyo nia ya kuanza mazungumzo juu
ya mkataba mpya na nyota huyo wa Argentina hivi karibuni.

Messi aliongeza mkataba wa miaka miwili na Barca mwezi Februari uliopita, ambapo mkataba wake na klabu unafika tamati hadi Juni 30, 2018, lakini mabingwa hao wa Kihispania wako tayari kujadili mkataba mpya na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26.

Bartomeu, ambaye alichukua majukumu ya urais wa klabu ya Barca  siku ya Alhamisi usiku kufuatia Sandro Rosell kujiuzulu ghafla , pia alionya hali ya uwezekano kwamba Messi hayuko katika soko, huku kukiwa na taarifa za mchezaji huyo kuzivutia klabu kubwa ikiwemo ya mabingwa wa kutumia wa Kifaransa, Paris Saint-Germain. 

Akizungumza na kituo cha redio cha Kikatalani,  RAC1, Bartomeu alisema: "Messi si kwa ajili ya kuuzwa". 

"Tunataka kukaa chini bila kurukaruka, na baba yake pamoja na wakala wake kwa sababu tunataka kuhakikisha kuwa yeye ni mchezaji bora ambaye analipwa kama anavyostahili."

Messi alifikisha mechi 400 akiwa na Barca wiki iliyopita katika robo-fainali ya kwanza  ya Copa del Rey  dhidi ya Levante na amefunga magoli 331 hadi sasa kwa klabu hiyo kubwa ya Kikatalani. 

Katika wakati wake akiwa Nou Camp, Messi alishinda Ballon d'Or rekodi mara nne, na vile vile kusaidia Barca kushinda vikombe kadhaa, ikiwa ni pamoja na Ligi kuu ya Spain mara sita, ​​Ligi ya Mabingwa mara tatu na Copa del Rey mara mbili.


 

Post a Comment

0 Comments