Kutokana na mgomo unaoendelea wa wafanyabiashara wa Kariakoo
naibu waziri wa fedha Mh Sada Salum amefafanua juu ya
utaratibu wa matumizi ya
mashine za kieletroniki[EFD] zenye lengo la kumrahisishia mfanyabiashara
kutunza kumbukumbu za biashara za kila siku ili kuondoa usumbufu wakati wa
ukadiriaji wa kodi
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es salam Mh Sada Salum amesema kuwa walengwa wa
mashine hizo ni wafanyabiashara wenye mauzo ya million 14 na zaidi wakiwemo:
-Wenye
maduka ya vipuri
-Mawakili
-Wenye
maduka ya jumla[sub wholesale shops]
-Migahawa mikubwa
-Migahawa mikubwa
-Wafanyabiashara
wakubwa wa mbao
-Maduka ya
simu na vipuri vyake
-Baa na vinywaji
baridi
-Studio za
picha
-:"Catering services"
-:"Catering services"
-Wauzaji wa
pikipiki
-Maduka
makubwa ya nguo
-Na biashara
zinginezo
| (kutoka kushoto)Naibu waziri wa fedha Mh Sada Salum na Mh.Janeth Mbene |
Aidha
Mamlaka ya mapato Tanzania imewataka wafanyabiashara na wadau mbalimbali kuwa
makini na matapeli wanaojifanya watumishi wa TRA ambao hupita madukani
kuwasumbua wafanyabiashara kuhusiana na matumizi ya mashine hizo, na endapo
watakutana na watu wa aina hiyo ni wajibu wa mwananchi kudai kitambulisho
ambacho nyuma huwa na namba ya mwajiri au kutoa taarifa kwa mamlaka husika.
Sanjari na
hayo Mh Sada Salum ametoa wito kwa wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa na
kuwasihi wafanyabiashara wakubwa ambao
hawataki kulipa kodi kuacha kuwashawishi na kuwachochea wafanyabishara wengine
kugoma kutumia mashine na kuwakumbusha kuwa KULIPA KODI STAHIKI NI WAJIBU WA
KILA MWANANCHI.
0 Comments