Chama
cha msalaba mwekundu (Tanzania Red Cross Society) kinazindua Mradi wa ugawaji
wa viatu kwa watoto wa shule na wa vituo vya kulelea watoto zaidi ya 500,000
kutoka Mikoa minane ya Tanzania.
![]() |
| Dr.George Nangale,ambaye ni Rais wa chama cha msalaba mwekundu |
Akizungumza na waandishi wa
habari Dr.George Nangale,ambaye ni Rais wa chama hiko,amesema Mikoa
itakayonufaika na mradi huu ni pamoja na Shinyanga, Tanga,
Mwanza, Tabora, Kilimanjaro, Pwani, Dar-es-Salaam na Zanzibar na kusema mradi huo utahusisha
Watoto wenye umri mdogo wasio jiweza kwani wengi wao wanaathirika na
magonjwa mbalimbali yanaosababishwa na
minyoo.![]() |
| Detha Mlaya ni mkurugezi wa Idara ya Afya |
Aidha
Dr.Nangale ameongeza kuwa, Viatu hivyo aina ya raba nyeusi, ni msaada kutoka
kampuni ya Toms Shoes, iliyoko Los Angeles Marekani, unaolenga watoto ambao
wazazi wao hawana uwezo wa kuwanunulia aina yoyote ya viatu, na kutoa wito kwa watanzania,kwamba viatu hivyo haviuzwi na havitakiwi kuuzwa
kwa watoto au wazazi wa watoto.
![]() |
| Dr.George Nangale akimvalisha viatu mmoja wa watoto waliohudhulia halfa hiyo |
![]() |
| Detha Mlaya ambae ni mkurugezi wa Idara ya Afya pia alimvalisha mtoto viatu hinyo |
Pia Dr.Nangale amesema Zaidi ya voluntia 1,000 kutoka Mikoa husika
wanajitolea katika shughuli hii ambayo ni pamoja na kubainisha walengwa, kuwasajili
na kugawa hivi viatu kuanzia wiki hii,na Mikoa iliyochaguliwa imezingatia uhai
wa chama na idadi ya voluntia mikoani humo.
![]() |
| Watoto wa shule ya msingi waliokuwepo katika halfa hiyo wakisubiri kuvalishwa viatu hivyo |
![]() |
| Baadhi ya wanahabari na wafanyakazi wa msalaba mwekundu wakifuatilia kinachojili |
“Vigezo vya
kuchaguliwa kwa mikoa hii ni kuwa ni sehemu ambapo Red Cross inatekeleza huduma za nyumbani
(Home Based Care) na miradi mingine.” Alisema
Dr. Nangale.
Red Cross,
katika shughuli hii inashirikiana kwa karibu na idara ya ustawi wa jamii na
MOHSW; Serikali za mitaa; Wakuu wa shule/vituo; Watendaji wa Kata, wazazi
husika, n.k. kuhakikisha watoto wasiojiweza na wasiokuwa na uwezo ndo
wananufaika na mpango huu.
Tanzania
Red Cross inatoa wito kwa
watanzania kwamba, viatu hivi haviuzwi na havitakiwi kuuzwa kwa watoto au
wazazi wa watoto.
Mratibu wa
mpango huu, Bi. Emma Msuya amesema
kwamba msaada huu wa viatu unatarajiwa kuwa wa miaka mitatu (3), ambapo kila
mwaka jozi zipatazo 1,000,000, zitatolewa kwa Tanzania na kampuni hiyo.
Msuya amesema
kampuni ya Tom Shoes imesha toa msaada huu wa viatu kwa nchi 43, Tanzania
ikiwemo kuanzia mwaka huu wa 2013. Baadhi ya nchi nyingine za kiafrika ambazo
zinapata msaada kama huu ni; Kenya, Zambia, Liberia na Malawi.
Tanzania
Red Cross inaomba Vyombo vya habari, serikali na wadau wote kusaidia katika
kuitaarifu jamii husika suala zima la mradi huu na kuhakikisha kwamba
walengwa wananufaika. Na pia kuhakikisha kwamba hamna mtu anaye ruhusiwa kuuza
au kununua aina ya viatu vinavyo gawiwa(Toms Shoes).






0 Comments