Ticker

6/recent/ticker-posts

ROMELU LUKAKU AUZA TIMU

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA AGOSTI 31,2013 SAA 9:00 USIKU
 Penalty  ya mwisho aliyokosa Romelu Lukaku imewapa ushindi Bayern Munich  katika Europa Super Cup  baada kupigwa  penalty
5-4.
Mchuano huo uliokuwa unakumbushia upinzani wa jadi wa makocha wapya wa timu hizo mbili yaani Chelsea na Bayern Munich, kwani Mourihno alikuwa mkufunzi wa Real Madrid huku Guardiola yeye akiwa na Barcelona zote za Uhispania,lakini katika mtanange huo Jose Mourihno(The happy one),aliondoka kichwa chini baada ya penalti ya mwisho.
Hasara: Lukaku inaonekana kushangaa baada ya kukosa penalty

Mabingwa tena: Bayern wanasheherekea ushindi baada ya Lukaku kukosa penalty 
Kiulaini: Javi Martinez (kulia) akiipatia Bayern bao la pili la kusawazisha katika dakika ya mwisho ya muda wa ziada.
 Bayern walifanikiwa kutwaa kombe hilo  baada ya kumaliza dakika 120 kwa kwenda sare ya mabao 2-2,ndipo zilipoamuliwa kupingwa penalty na Bayern wakashinda kwa penalty 5 kwa 4 za Chelsea.
Katika mchezo Walioanza kupata bao walikuwa ni Chelsea kupitia kwa Fernando Torres katika dakika ya 8 ndani ya kipindi cha kwanza,kisha wachezaji wakaenda mapumziko Chelsea wakiwa wanaongoza kwa bao 1 kwa0.Baada ya mapumziko katika dakika ya 47 Franck Ribéry akaisawazishia Bayern,lakini Chelsea walimaliza dakika 90 wakiwa  pungufu baada ya Ramires kupewa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 85 baada ya kumchezea vibaya Mario Gotze,na dakika 90 zikawa zimemalizika kwa timu hizo kufungana bao 1 kwa 1.kisha zikaongezwa dakika 30.
Eden Hazard,akiipatia bao la pili Chelsea ndani ya muda wa ziada katika dakika ya 93,na kuifanya timu hiyo kujipa matumaini ya kuondoka na kombe hilo,kwani mpaka dakika 30 za ziada zinakaribia kuisha timu Bayern bado wakiwa hawajasawazisha japo kuwa waliutawala mchezo ndani ya dakika hizo,lakini bayarn walizidi kuzinduka na kuwafanya Chelsea kuzidi kuwa na hofu na hatimaye wakaweza kusawazisha bao la pili kupitia kwa Javier Martinez katika dakika moja ya ziada iliyoongezwa,kwani pia dakika 120 zilikuwa zimeshakwisha.
Hazard akipachika bao la pili kwa upande wa Chelsea
Kabla:Hazard akiiwezasha Chelsea kuongoza kwa bao 2-1 katika muda wa ziada
Nenda nje:: Ramires akipewa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 85 baada ya kumchezea vibaya Mario Gotze
Kisha mwamuzi akaamua Penalty zipigwe,na kwa upande wa Bayern waliopata penalty ni David Alaba,Toni Kroos,Philipp Lahm,Franck Ribéry na Xherdan Shaqir.
Kwa upande wa Chelsea waliopata penarty ni David Luiz,Oscar,Frank Lampard na Ashley Cole,na aliyekosa alikuwa ni mchezaji kinda aliyetokea kuwa mashuhuri tangu msimu uliopita akiwa kwa mkopo West Bromwich Albion, Romelu Lukaku ndiye aliyekosa penati na kupeleka kombe hilo Ujerumani.
Kutoka nyuma: Ashley Cole wa Chelsea na Arjen Robben kwenye vita kwa ajili ya mpira
To,to,to,to,toTorres,akiipatia bao la kwanza Chelsea
Franck Ribery wa  Bayern alifunga  baada ya kipindi cha pili katika dakika ya 47
Uwanja ulitapika:mashabiki wa Bayern wakipeperusha bendera kabla ya mchezo
Mbwatukaji: Mourinho,hatulii kama kawaida yake
Asanteeee: Ribery alikwenda moja kwa moja,kwa bosi wa Bayern Pep Guardiola baada ya kufunga bao la kusawazisha
Uwanja mpya:uwanja wa Edeni,ndio uliotumika kwa ajili ya fainali hiyo
Kikosi cha Bayern Munich: Neuer, Rafinha (Javi Martinez 56), Dante, Boateng, Alaba, Muller (Gotze 70), Lahm, Kroos, Ribery, Mandzukic, Robben (Shaqiri 95).

Wachezaji wa akiba: Starke, Van Buyten, Contento, Pizarro.

Kadi ya njano: Ribery

wafungaji: Ribery (47), Javi Martinez (120)

Kikosi cha Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Luiz, Cole, Ramires, Lampard, Hazard, Oscar, Schurrle, Torres (Lukaku 97).

Wachezaji wa akiba: Schwarzer, Azpilicueta, Terry, Essien, Mikel, Mata.

Kadi za njano: Cahill, Ramires, Luiz, Torres, Cole, Ivanovic

Kadi nyekundu: Ramires (84)

Wafungaji: Torres (8) Hazard (93)




.




Post a Comment

0 Comments