Ticker

6/recent/ticker-posts

GARETH BALE:REAL MADRID WAKUBALIANA MASLAHI BINAFSI


Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA AGOSTI 30,2013 SAA 2:00 USIKU


Gareth Bale imekubali kufikia makubaliano kuhusiana na maslahi binafsi ya kujiunga na klabu ya  Real Madrid,kuelekea usajili
utakaovunja rekodi ya dunia  kutoka katika klabu yake ya  Tottenham.
 Hata hivyo, klabu ya Real madridi bado iko katika  majadiliano juu ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 , kwa jitihada  za fedha ya £ 86m ambayo   tayari imewasilishwa kwa Spurs.
Mwandishi mkuu wa habari za michezo kutoka shirika la habari la BBC Dan Roan,amesema Makubaliano juu ya suala binafsi,hakuna kizuizi juu ya hilo, na wakati mazungumzo yaliyochukuwa siku kazaa  na  Madrid,kulikuwa hakuna kikwazo kuhusiana na swala hilo.
Cristiano Ronaldo:Rekodi yake inatarajiwa kuvunjwa
Iwapo Spurs watakubali rasmi ofa hiyo ya Real Madrid ,basi ofa hiyo itakuwa ni ya rekodi ya dunia,na kuishinda ile waliyopewa Manchester United ya £ 80m mwaka 2009 kwa Cristiano Ronaldo kwenda Real Madrid.

Post a Comment

0 Comments