Ticker

6/recent/ticker-posts

Simba Sc imeifanya Tff Kuweka Utaratibu huu

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA 10,SEPT.2018 SAA 03:17 USIKU


Shirikisho la soka nchini TFF limewakumbusha wanachama wake juu ya mpango wa kuzialika timu kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kucheza michezo ya
kirafiki ama kushiriki michuano ya soka.
TFF wamewakumbusha wnaachama wake suala hilo, kufuatia ujio wa klabu ya AFC Leopard kutoka nchini Kenya iliyocheza na Simba mwishoni mwa juma lililopita jijini Dar es salaam, kuwa na ukakasi.
Mualiko mwingine ambao ulikua na ukakasi ni ile ulioihusisha klabu ya Sonny Sugar ambayo ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Biashara United mkoani Mara.
Mkurugenzi wa mashindano wa shirikisho hilo Salum Madadi amesema kuna ulazima kwa wanachama wa TFF wakajikumbusha utaratibu uliopo kisheria wa kuzialika timu kutoka nje ya nchi na kucheza michezo wa kirafiki ya kimataifa, ili kutambua nafasi zao chini ya mwamvuli wa mamlaka ya soka nchini.
 Bofya chini Kusikiliza
..>>>..

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo),na instagram- kihwiliupdates

Post a Comment

0 Comments