Shirikisho la soka nchini TFF, limetoa muda wa siku mbili
kwa viongozi wa Young Africans kuwasilisha sababu kwa njia ya
maandishi (barua) za kushindwa kukamilisha zoezi la usajili wa wachezaji kwa njia ya TMS kama kanuni za ligi kuu ya soka Tanzania bara zionazotaka.
maandishi (barua) za kushindwa kukamilisha zoezi la usajili wa wachezaji kwa njia ya TMS kama kanuni za ligi kuu ya soka Tanzania bara zionazotaka.
TFF juzi walithibitisha hawajapokea usajili wa wachezaji wa
Young Africans kwa njia ya mtandao, halia mbayo huenda ikawasababishia matatizo
makubwa kutoka FIFA, likiwepo suala la kushushwa daraja.
Katibu mkuu wa TFF Celestine Mwesigwa, hii leo amekutana na
waandishi wa habari na kusema kwamba sababu za kimaandishi ambazo
zitawasilishwa na mabingwa hao wa Tanzania bara ndizo watakazo zitumia kwa
ajili ya kuwaombea utetezi FIFA, ili kuona kama watapata uwezekano wa
kufunguliwa kwa mtandao wa usajili wa wachezaji ambao tayari umeshafungwa tangu
usiku wa kuamkia jumapili.
Mwesigwa amesema mbali na Young Africans pia zipo klabu
nyingine za ligi daraja la kwanza (Coastal Union) ambazo zimeshindwa kutimiza masharti ya
kikanuni ya kufanya usajili wa wachezaji wakati wa dirisha la usajili ambalo
lilifunguliwa rasmi June 15 na kufungwa Agosti 06.
Hivyo sasa klabu zote ambazo hakuzituma usajili
wake, hazina budi kuandaa utetezi utakaokwenda TFF ambao utatumwa FIFA
yenye mamlaka ya kufungua dirisha, na utetezi huo ukikataliwa timu
husika inabidi ishuke daraja ambalo halimo kwenye usajili wa mfumo wa
TMS.
TFF kwa sasa inasuburi barua ya utetezi wa klabu
ambazo hazikukamilisha zoezi la usajili ili iutume FIFA. Sambamba na
hilo TFF inatathimini mwenendo mzima kisha itatoa taarifa kwa FIFA ili
kuangalia namna gani ya kushughulikia maeneo yaliyokuwa na upungufu kwa
sasa na baadaye.

0 Comments