Aliyekuwa nahodha wa Simba SC, Mussa Hassan Mgosi hii leo AUG 14,2016 amewaaga rasmi mashabiki wa klabu ya simba baada
ya kustaafu rasmi soka .
Mgosi alitumia nafasi hiyo kuwaaga mashabiki katika mchezo wa kirafiki wa Simba Dhidi ya URA mchezo uliomalizika kwa sare ya Bao 1 - 1 uliopigwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mgosi aliyeungana na familia yake kusheherekea mafanikio yake yake na Simba,alicheza dakika tatu za kipindi cha kwanza kabla ya nafasi yake kuchukuliwa na Jamal Mnyate.kipindi anatoka Mgosi aliinama na kuubusu mpira,kisha akavua kitambaa cha unahodha na kumpatia Jonas Mkude.
Mgosi kwa sasa anakuwa Meneja wa Simba SC.
Mabao yote yalifungwa kipindi cha kwanza,bao la URA lilipatikana dakika ya 19 kupitia kwa Nkugwa Eklanah na bao la kusawazisha la Simba SC likifungwa dakika ya 32 na Nahodha mpya, Jonad Gerald Mkude
ANGALIA PICHA
0 Comments