Ticker

6/recent/ticker-posts

AUDIO:JUMA PONDAMALI KUACHANA NA YANGA ? ..msikilize hapa akifunguka...

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.AUG 3,2016 SAA 11:43 JIONI
Watatu kutoka kulia:kocha wa makipa wa Yanga Juma pondamali
Aliyekua mlinda mlango wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania  juma Pondamali huenda akaachana na klabu ya Young Africans
ambayo ameitumikia katika nafasi ya kocha wa makipa kwa miaka kadhaa.

Pondamali amethibitisha kuwa tayari kuondoka klabuni hapo, kufuatia mkataba wake kufikia kikomo na mpaka sasa hakuna mazungumzo yoyote yanayoendelea kati yake ya uongozi wa Young Africans.

Amesema endapo itatokea suala la yeye kushindwa kupewa mkataba mpya ndani klabu hiyo kongwe, atajielekea katika klabu nyingine ambayo tayari imeshaonyesha nia ya kutaka kufanyanae kazi.

MSIKILIZE JUMA PONDAMALI
Hata hivyo pondamali amesema hana mpango wa kuwa na ndoto za kutoka nje ya nchi na kwenda kusaka kazi ya kuwa kocha wa makipa katika timu za taifa ama klabu, kutokana na kuwa na kiu ya kutaka kuwanyanyua watanzania.


Wakati huo huo Pondamali akazungumzia kozi ya makocha ambayo anashirikishi kwa kusema inaendelea kumuongezea ujuzi na anaamini hata washiriki wenzake wananufaika na mafunzo wanayoyapata.

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

Post a Comment

0 Comments