Siku ya Tarehe 11 mwezi huu April 2015 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Kikosi cha wakongwe wa Barcelona na nyota
wakongwe wa Tanzania walicheza mechi ya kirafiki,mchezo huo uliokosa watazamaji wakutosha ulimalizika kwa Kikosi cha wakongwe wa Barcelona kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya nyota wakongwe wa Tanzania.
Dakika 45 za kwanza timu zilikwenda mapumziko zikiwa zimefungana bao 1-1,Barcelona walikuwa wa kwanza kufunga bao kupitia kwa Luis Garcia ambaye aliwachambua mabeki wa Tanzania wakongwe na kufunga. Yusuf Macho ‘Musso’ akafunga baso safi la pili kwa shuti kali katika dakika ya 42.
Kipindi cha pili Balcelona walipata bao la ushindi dakika za mwishoni kabisa baada Patrick Kluivert kufunga mkwaju wa penalti uliomuacha kipa Juma Kaseja akianguka kushoto kwake na mpira ukiingia kulia,na mpira kumalizika Barcelona 2 - 1 Tanzania.
ANGALIA PICHA ZA MCHEZO
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) .














































0 Comments