Ticker

6/recent/ticker-posts

POLISI WA GHANA KUCHUNGUZA KIFO CHA MWAMUZI WA NCHINI HUMO

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 12,2014 SAA 11:46 JIONI

Polisi nchini Ghana wameanzisha uchunguzi wa kifo cha mwamuzi msaidizi wa mpira wa miguu, ambaye ameripotiwa kudhalilishwa
kwa kupigwa vibaya, baada ya kutoa maamuzi ya utata katika mechi ya ligi ya ndani nchini humo, msemaji wa polisi nchini humo amesema hii leo Jumatano.

Kwame Andoh Kyei, ambaye alifariki siku ya Ijumaa, alikuwa mwamuzi msaidizi katika mechi ya daraja la pili, iliyopingwa katika mji wa magharibi wa Bordie Machi 2.

Msemaji wa chama cha mpira cha Ghana, Ibrahim Sannie Daara alisema Kyei ilidhalilishwa baada ya uamuzi wa utata,lakini hakuwai mara moja kutafuta matibabu. 

Olivia Adiku, msemaji wa polisi katika mkoa wa magharibi, alisema wapelelezi walikuwa wakisubiri maelezo ya uchunguzi ambayo yanaweza kuja wiki hii. 

 Ilikuwa  wazi kuwa mwamuzi Kyei alikufa kutokana na majeraha endelevu wakati wa mechi, aliongeza Olivia Adiku,ambaye ni msemaji wa polisi katika mkoa wa magharibi. 

"Kwa sasa, hatuwezi kusema kama ni timu iliyokuwa nyumbani ambao walimshambulia au timu ya ugenini," Daara aliiambia AFP. 

Polisi ni kawaida hutoa usalama katika mechi maalumu katika mkoa wa magharibi lakini hawakuwepo Machi 2 kwa sababu klabu "hawakuweza kuomba kibali kwa ajili ya usalama fulani", alinukuliwa Adiku akisema. 

Alisema kutokea kwa vurugu zinazohusisha mpira ni nadra sana katika eneo hilo.

Post a Comment

0 Comments