Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA FEB. 7,2014 SAA 02:19 JIONI
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linazitakia kila la kheri klabu za Yanga na
Azam ambazo timu zake
zinatuwakilisha kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa
Afrika (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).
Yanga
inacheza na Komorozine ya Comoro katika mechi ya kwanza ya raundi ya awali ya
CL itakayochezwa kesho (Februari 8 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kuanzia saa 10 kamili jioni.
Nayo
Azam inaikaribisha Ferroviario de Beira ya Msumbiji katika mchezo wa kwanza wa
raundi ya awali ya CC utakaochezwa Jumapili (Februari 9 mwaka huu) saa 10
kamili kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
Ni
matumaini yetu kuwa timu hizo mbili zitatuwakilisha vizuri kwenye michuano hiyo,
na kuwataka Watanzania wajitokeze kwa wingi viwanjani kuziunga mkono hasa kwa
vile zinacheza nyumbani.
TWIGA STARS
YAHAMISHIA KAMBI DAR
Timu
ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) imehamishia kambi yake
jijini Dar es Salaam kutoka Mlandizi mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi
ya mechi ya michuano ya Afrika (AWC) dhidi ya Zambia.
Kikosi
hicho chini ya Kocha Rogasian Kaijage kimepiga kambi katika hosteli ya Msimbazi
Center kikiwa na wachezaji 25 kutoka 30 ambao kilianza nao katika kambi ya
Mlandizi mkoani Pwani.
Mechi
hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza dhidi ya Zambia itachezwa Februari 14 kwenye
Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka. Timu zitarudiana wiki mbili baadaye jijini Dar
es Salaam.
Wachezaji
waliopo katika kikosi hicho ni Amina Ally, Amisa Athuman, Anastasia Anthony, Asha
Rashid, Esther Chabruma, Eto Mlenzi, Evelyn Sekikubo, Fatuma Bashiri, Fatuma
Hassan, Fatuma Issa, Fatuma Mustafa na Fatuma Omari.
Wengine
ni Flora Kayanda, Happiness Hezron, Maimuna Said, Mwajuma Abdallah, Mwapewa
Mtumwa, Najiat Abbas, Pulkeria Charaji, Shelder Boniface, Sophia Mwasikili,
Therese Yona, Vumilia Maarifa, Winfrida Daniel na Zena Khamis.

0 Comments