Ticker

6/recent/ticker-posts

TAARIFA KUHUSU TWIGA STARS PAMOJA NA YA TFF KUZITAKIA KILA LA KHERI YANGA NA AZAM

 Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA FEB. 7,2014 SAA 02:19 JIONI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linazitakia kila la kheri klabu za Yanga na Azam ambazo timu zake
zinatuwakilisha kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).

Yanga inacheza na Komorozine ya Comoro katika mechi ya kwanza ya raundi ya awali ya CL itakayochezwa kesho (Februari 8 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Nayo Azam inaikaribisha Ferroviario de Beira ya Msumbiji katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali ya CC utakaochezwa Jumapili (Februari 9 mwaka huu) saa 10 kamili kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

Ni matumaini yetu kuwa timu hizo mbili zitatuwakilisha vizuri kwenye michuano hiyo, na kuwataka Watanzania wajitokeze kwa wingi viwanjani kuziunga mkono hasa kwa vile zinacheza nyumbani.

TWIGA STARS YAHAMISHIA KAMBI DAR
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) imehamishia kambi yake jijini Dar es Salaam kutoka Mlandizi mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya michuano ya Afrika (AWC) dhidi ya Zambia.

Kikosi hicho chini ya Kocha Rogasian Kaijage kimepiga kambi katika hosteli ya Msimbazi Center kikiwa na wachezaji 25 kutoka 30 ambao kilianza nao katika kambi ya Mlandizi mkoani Pwani.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza dhidi ya Zambia itachezwa Februari 14 kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka. Timu zitarudiana wiki mbili baadaye jijini Dar es Salaam.

Wachezaji waliopo katika kikosi hicho ni Amina Ally, Amisa Athuman, Anastasia Anthony, Asha Rashid, Esther Chabruma, Eto Mlenzi, Evelyn Sekikubo, Fatuma Bashiri, Fatuma Hassan, Fatuma Issa, Fatuma Mustafa na Fatuma Omari.

Wengine ni Flora Kayanda, Happiness Hezron, Maimuna Said, Mwajuma Abdallah, Mwapewa Mtumwa, Najiat Abbas, Pulkeria Charaji, Shelder Boniface, Sophia Mwasikili, Therese Yona, Vumilia Maarifa, Winfrida Daniel na Zena Khamis. 

Post a Comment

0 Comments