IMEWEKWA FEB. 13,2014 SAA 10:42 JIONI
Mshambuliaji wa kimataifa wa timu ya Uganda na timu ya Young Africans
 leo ameruhiswa ramsi kuanza kuitumikia timu yake katika 
michezo ya Ligi
 Kuu na Mashindano ya klabu Bingwa Barani Afrika kufuatia shirikisho la 
soka nchini TFF kuiandikia barua klabu ya Young Africans.
Okwi ambaye alisajiliw aa Young Africans mwishoni mwa mwaka jana na 
kucheza michezo ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya, alisimamishwa na
 Shirikisho la Soka la Nchini TFF wakati wakisubiria kupata udhibitisho 
wa usajili wake kutoka FIFA.
Mara baada ya barua hiyo, Okwi 
anatarajiwa kuungana na wenzake mwishoni mwa wiki mara timu itakaporejea
 kutoka Visiwa vya Comoro na ataanza kuonekana katika mchezo wa Ligi Kuu
 ya Vodacom dhidi ya Ruvu Shooting siku ya jumamosi Februari 22 mwaka 
huu.
Uongozi wa Young Africans 
unawashukuru wanachama, wapenzi na wadau kwa ujumla kwa kuwa wavumilivu 
wakati wa suala na hili na hatimaye limepatiwa ufumbuzi.
CHANZO:www.youngafricans.co.tz 

 
 
0 Comments