Ticker

6/recent/ticker-posts

HII NDIYO ZAWADI AMBAYO ROBERT LEWANDOWSKI ANATAKA KUWAPA MASHABIKI WA DORTMUND KABLA YA KUONDOKA

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 6,2014 SAA 12:35 ASUBUHI
Robert Lewandowski  amefafanua malengo yake ya mwisho akiwa katika kikosi cha Borussia Dortmund  kuwa anataka kushinda
kikombe cha mwisho kabla ya kuhamia rasmi katika klabu ya Bayern Munich msimu huu.

BVB sasa wako nyuma kwa alama 17 kwa Bayern ambao ndio viongozi wa ligi hiyo ya Bundesliga na wana uwezekano wa kuwa mabingwa wa ligi hiyo kwa muda huu.

Hata hivyo, Dortmund bado wana nafasi ya kushinda kumbe  kuu kama watafanikiwa raundi ya 16 ya Ligi ya Mabingwa, ambapo wao watakutana na Zenit St Petersburg, na DFB Pokal katika robo fainali, ambayo watawasubiri Eintract Frankfurt.  

"Lengo langu bado ni kuondoka Borussia Dortmund na kikombe msimu huu wa majira ya joto," Lewandowski alinukuliwa akisema na Sport Bild. 

"Lakini sisi sote tunajua tunatakiwa kuboresha. Bila shaka, tulikuwa na wachezaji wengi majeruhi, lakini wote walipoona na timu inatakiwa kushinda kila mchezo".

"Watu wengi wanadai kwamba mimi sina nia tena ya kucheza katika timu ya Dortmund, lakini mimi ninaonyesha kuwa bado nina nia ya kucheza kwa BVB. Nataka kuwapa mashabiki  zawadi nzuri ya kuwaaga."   

Lewandowski ametikisa nyavu mara 11 katika mechi 19 za Bundesliga alizoshiriki msimu huu, lakini bado hajafunga tangu kutangaza uhamisho wake kwenda Bayern. 

Post a Comment

0 Comments