Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 14,2014 SAA 06:01 USIKU
David
 Moyes anaona timu yake ya Manchester United bado iko katika vita kwa ajili ya kugombea nafasi nne za juu katika ligi kuu 
ya Barclays  baada ya kutoka sare ya bila kufungana na timu ya Arsenal.
Nafasi walikuwa nayo katika Ligi kuu,ambayo imeshindwa kuwapandisha,  matokeo yake imezidi kuibakisha kileleni Chelsea katika msimamo.
United
 ingeweza pia kuondoka  London kaskazini na ushindi kama si kipaji 
cha kuokoa mikwaju kutoka Wojciech Szczesny, ambaye alisukuma nje makombola kutoka kwa Robin van
 Persie .
United, wametolewa nje ya Kombe la FA katika raundi ya tatu,na sasa watakuwa na 
mapumziko ya mazoezi huko Dubai kabla ya kuanza kwa hatua ya Ligi Kuu kwa kupambana na 
Crystal Palace Februari 22.
"Ninachoweza kufanya -na kuendelea kusema - ni sisi kujaribu na kushinda mchezo ujao na kujiweka juu," alisema Moyes. 
"Kama
 kuna klabu moja katika historia ambao wamekuwa na nguvu ya kushinda 
michezo katika nusu ya pili ya msimu na kuweza kuleta pressure kwa timu za 
juu, ni Manchester United.Tutaendelea kujaribu na kufanya hivyo na 
kufanya kazi yetu."
"Tunaweza kufanya kazi yetu bora, tunaweza,tunataka kucheza vizuri,hatuwezi kusumbua timu nyingine,tunaweza tu kuleta  pressure na 
kushinda michezo yetu."
Moyes aliongeza: "Naamini hamu bado ipo katika kikosi". 

 
 
0 Comments