Ticker

6/recent/ticker-posts

DAVID MOYES:MANCHESTER UNITED BADO INA NJAA YA KUPIGANIA NAFASI NNE ZA JUU YA LIGI KUU

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 14,2014 SAA 06:01 USIKU
David Moyes anaona timu yake ya Manchester United bado iko katika vita kwa ajili ya kugombea nafasi nne za juu katika ligi kuu
ya Barclays  baada ya kutoka sare ya bila kufungana na timu ya Arsenal.

Nafasi walikuwa nayo katika Ligi kuu,ambayo imeshindwa kuwapandisha, matokeo yake imezidi kuibakisha kileleni Chelsea katika msimamo.

United ingeweza pia kuondoka  London kaskazini na ushindi kama si kipaji cha kuokoa mikwaju kutoka Wojciech Szczesny, ambaye alisukuma nje makombola kutoka kwa Robin van Persie .

United, wametolewa nje ya Kombe la FA katika raundi ya tatu,na sasa watakuwa na mapumziko ya mazoezi huko Dubai kabla ya kuanza kwa hatua ya Ligi Kuu kwa kupambana na Crystal Palace Februari 22.

"Ninachoweza kufanya -na kuendelea kusema - ni sisi kujaribu na kushinda mchezo ujao na kujiweka juu," alisema Moyes. 

"Kama kuna klabu moja katika historia ambao wamekuwa na nguvu ya kushinda michezo katika nusu ya pili ya msimu na kuweza kuleta pressure kwa timu za juu, ni Manchester United.Tutaendelea kujaribu na kufanya hivyo na kufanya kazi yetu."

"Tunaweza kufanya kazi yetu bora, tunaweza,tunataka kucheza vizuri,hatuwezi kusumbua timu nyingine,tunaweza tu kuleta  pressure na kushinda michezo yetu."

Moyes aliongeza: "Naamini hamu bado ipo katika kikosi".
   

 

Post a Comment

0 Comments