Ticker

6/recent/ticker-posts

CARDIFF CITY WAMCHUKUA FABIO NA JONES,LAKINI PIA KUMALIZANA NA ZAHA NDANI YA MASAA 24

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA JANU. 28,2014 SAA 07:45 USIKU

Cardiff City wamemsaini mchezaji wa Manchester United ambaye ni raia wa Brazil  Fabio na mshambuliaji wa  Stoke City  Kenwyne
Jones, meneja wa klabu hiyo ya Ligi Kuu  Ole Gunnar Solskjaer alisema siku ya Jumatatu.

Cardiff pia wana matumaini ya kumuajiri winga wa Manchester United Wilfried Zaha kwa mkopo kabla ya mwisho wa dirisha dogo la uhamisho siku ya Ijumaa.

"Fabio na Kenwyne wataungana na katika mazoezi siku ya leo,nimekutana nao na kwamba na hii ni zaidi ya kile tunachokifanya," Solskjaer aliwaambia waandishi wa habari huko Manchester kabla ya mchezo wa  Ligi Kuu dhidi ya United siku ya Jumanne. 

Solskjaer ambaye ni raia wa Norway , ambaye pia amechukua majukumu ya kuinoa Cardiff mwezi huu, alisema mpango wa Zaha ilikuwa bado haujakamilika. 

"Tunatumaini kufanikisha jambo hilo katika masaa 24 yajayo au hivyo, ili aweze kuwa tayari kwa ajili ya mwishoni mwa wiki,"mshambuliaji  huyo wa zamani wa Manchester United alisema. 

Cardiff katika msimamo ipo katika nafasi ya chini kabisa na iko katika hatari ya kushushwa daraja kufuatia kupanda daraja katika Ligi Kuu kwa mara ya kwanza mwaka jana. 

Post a Comment

0 Comments