Bodi
ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) imefungia viwanja saba vilivyokuwa
vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza
(FDL) hadi
vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi za
mpira wa miguu.
Uamuzi
huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika
juzi (Novemba 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo
mengine kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katika mzunguko wa
kwanza.
Viwanja
vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza ili
viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa
yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji), na Uwanja wa
CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo
(dressing rooms) havina hadhi).
Uwanja
wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea- pitch ni
mbovu), Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha
(pitch ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia
kutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea
(pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu).
Klabu
ambazo timu zake zinatumia viwanja hivyo zimeshaarifiwa rasmi juu ya
uamuzi huo ambapo ama vinatakiwa kuwasiliana na wamiliki wa viwanja
hivyo ili wafanye marekebisho au kutafuta viwanja vingine vya kuchezea
mechi zao.
(UNARUHUSIWA KUSHARE HABARI HII KWA MARAFIKI ZAKO)
(UNARUHUSIWA KUSHARE HABARI HII KWA MARAFIKI ZAKO)

0 Comments