Ticker

6/recent/ticker-posts

KOMBE LA DUNIA:FIFA YAJIBU MADAI YA KUKIUKA HAKI ZA BINADAMU KWA WAFANYAKAZI

 Mhariri:Herman Kihwili.IMEWEKWA NOVEMBA 18.2013 SAA 12:06 JIONI
FIFA imejibu madai yaliyotolewa shirika la haki za binadamu Amnesty International, juu ya kuwanyanyasa  wafanyakazi wa
kigeni" nchini Qatar na kusisitiza wao wanafuata haki ya kijamii kwa wale wanaohusika katika miradi ya World Cup.
Amnesty walitoa ripoti yenye kurasa 166 wakida kwamba  wafanyakazi waliosalia nchini Qatar kwa kazi za miradi ya ujenzi kuhusiana na Kombe la Dunia 2022 wanakabiliwa na "malipo yasiyo ya haki kwa mishahara,na hatari ya mazingira ya kazi,pamoja na viwango vikubwa na vya kutisha vya malazi"
Katibu mkuu wa Amnesty International  Salil Shetty ilisema kuwa "ni kiwango cha kutisha cha unyonyaji katika sekta ya ujenzi nchini Qatar. 
Viongozi hao wa soka Ulimwengu walijibu kwa kusisitiza kuwa,wao huchukulia masuala hayo kwa umakini sana na kuthibitisha kuwa wao wanafanya kazi kwa ukaribu na mamlaka ya nchini Qatari kushughulikia hali hiyo. 
"FIFA inafanya kazi wazi na kuheshimu haki za binadamu na matumizi ya kanuni za kimataifa kama kanuni ya shughuli zetu zote," taarifa rasmi ya FIFA Ilisema.
Na kuongeza kuwa "FIFA inaelewa na kushirikiana kwa juhudi na Amnesty International, kulinda haki ya kijamii na kuheshimu haki za binadamu,hasa kwa ajili ya dini na madhumuni ya FIFA". 
"FIFA pia anatarajia kuwa mwenyeji wa mashindano yake kikamilifu kuheshimu hayo yote Kama matokeo, na rais wa FIFA Blatter binafsi alitembelea Qatar tarehe 9 Novemba Alitoa dhamira imara ya kuwa mwenyeji 2022.

Post a Comment

0 Comments