Mhariri:Herman Kihwili.IMEWEKWA NOVEMBA 18.2013 SAA 02:56 USIKU
Mshambuliaji wa England
Daniel Sturridge anatia mashaka juu ya mechi ya kirafiki siku Jumanne dhidi ya
Ujerumani katika uwanja
wa Wembley baada ya kuondoka mapema katika mazoezi leo
Jumatatu.
Mchezaji huyo amefanya mazoezi kwa dakika 45 siku ya leo Jumatatu asubuhi kabla ya kuondoka uwanja.
Mchezaji huyo wa Liverpool mwenye umri wa miaka 24 alikosa katika mechi ya kirafiki kwa sababu ya kuumia mguu, ambao walifunngwa na chile mabao 2 kwa 0 siku ya ijumaa .
Lakini Daniel Sturridge na Kyle Walker wamethibitisha wao wako fit kwa ajili ya mechi dhidi ya Ujerumani siku ya Jumanne.
Mchezaji wa Tottenham
Walker, 23, pia alikosa kucheza katika mechi kadhaa kwa
sababu ya tatizo misuli.
Wakati huo huo, Muingereza beki Phil Jones atakosa katika mchezo huo kwa sababu ya tatizo la mafindofindo.
Lakini
bosi wa England Roy Hodgson ana matumaini anaweza kuwaita baadhi ya wachezaji
ambao walikosa mchezo wa Chile na kuwapa nafasi katika mechi dhidi ya timu kali
ya Ujerumani, ambao ni wa pili katika viwango vya Fifa vya dunia,nafasi nane
juu ya England.
0 Comments