Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMA WEWE NI SHABIKI WA MPIRA WA KIKAPU,TAARIFA HII INAKUHUSU

 Na.Richard Jules,IMEWEKWA NOV. 14,2013 SAA 10:30 JIONI

TAARIFA YA KUSOGEZWA MBELE LIGI YA MPIRA WA KIKAPU MKOA WA DSM (RBA) 2013/14.

Ndugu Wadau wa Mpira wa KIKAPU Mkoa DSM.

Napenda kuchukua nafasi hii kwa mara nyingine kuwataarifu juu ya kusogezwa mbele kwa Mashindano ya Ligi ya Mpira wa KIKAPU Mkoa wa Dar Es Salaam (RBA) kwa msimu wa mwaka 2013/14 yaliyokuwa yakitarajiwa kuanza siku ya Jumamosi tarehe 16/11/2013.

Chama Cha Mpira wa Kikapu mkoa wa Dar Es Salaam (BD), baada ya kikao chake cha Bodi kilichokaa na kutathmini mawazo mbalimbali toka kwa Viongozi na wadau mbalimbali waliohudhuria Mkutano Maalumu ulioandaliwa na Chama na wadau wa mpira wa Kikapu DSM yenye nia ya kuongeza Tija katika mchezo wetu ngazi ya Mkoa, kimefikia Azimio la kusogeza mbele kwa mashindano ya RBA kwa msimu huu 2013/14 mpaka hapo itakapotangazwa tena.

Barua za Taarifa hizi zimekwisha fika Vilabuni na mchakato wa kuzisambaza unaendelea.

Sambamba na hilo.

Viongozi wote wa Vilabu shiriki Ligi ya Mkoa (RBA) 2013/14 mnaombwa kufika bila kukosa katika Mkutano wa Viongozi wote siku ya Jumanne tarehe 19/11/2013 kuanzia saa 10:00 jioni katika Ukumbi wa Taasisi ya Malezi ya Vijana ya DON BOSCO – Upanga.

BD inaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza tokana na mabadiliklo hayo, ambayo kimsingi yamezingatia matakwa ya wadau wa Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar Es Salaam ili kuweza kuleta Tija katika kuendeleza jitihada za kuboresha Mchezo wa Mpira wa Kikapu Mkoani na Taifa kwa ujumla.

BD inatambua na kuthamini michango wa wadau na Ushirikiano utakaoleta ufanisi katika maendeleo ya mchezo wa Mpira Kikapu Mkoa wa Dar Es Salaam.

IMETOLEWA NA:

Richard Jules.
MAKAMU WA RAISI-BD.
CHAMA CHA MPIRA WA KIKAPU DSM (BD)

Post a Comment

0 Comments