IMEWEKWA OCTOBA 13,2013 SAA 02:13USIKU
Raundi
ya tisa ya ligi kuu Tanzania bara imeendelea hii leo Jumapili (Oktoba 13 mwaka huu)
kwa mechi nne katika
viwanja vinne tofauti.
Mchezo wa kwanza ulikuwa ni kati ya Ruvu Shooting na Rhino Rangers,mchezo uliopingwa katika uwanja wa Mabatini Mlandizi,mchezo huo umemalizika kwa timu ya Ruvu Shooting kuibuka na ushindi wa bao 1 kwa 0,bao pekee la timu hiyo liliwekwa nyavuni na Elius Maguri katika dakika ya 77.
Mgambo Shooting na Mbeya City walikipiga katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga,mchezo uliomalizika kawa timu ya Mbeya City kuendeleza ubabe baada ya kuitandika Mgambo Shooting bao 1 kwa 0,bao pekee lililowekwa nyavuni na Jeremiah John ndani ya dakika ya 20.
Azam Fc wanarambaramba au matajiri wa bongo walikuwa wakipambana na JKT Ruvu katika uwanja wao wa Azam
Complex jijini Dar es Salaam,mchezo uliomalizika kwa azam Fc kuibamiza timu ya JKT Ruvu mabao 3 kwa 0.Mabao ya Azam Fc yalifungwa na John Bocco ‘Adebayor’ dakika ya 12, beki Erasto Nyoni dakika ya 39 na kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ dakika ya 90.
Katika uwanja wa Manungu,
Turiani wenyeji Mtibwa Sugar walikuwa wakikipiga na Oljoro JKT,mchezo uliomalizika klwa timu ya Mtibwa Sugar kuimuka na ushindi wa bao 5 kwa 2,Mabao matatu ya ya Mtibwa yalifungwa na Abdallah Juma katika dakika ya 23, 66 na 78.Na mabao mawili yalifungwa na Juma Luizio dakika ya 5 na 31.
Na mabao ya Oljoro yamefungwa na Shaibu Nayopa dakika ya 72,na kwa mkwaju wa penalti, Amir Omar akaipatia Oljoro bao la pili katika dakika ya 84.

0 Comments