Ticker

6/recent/ticker-posts

MESUT ÖZIL AMESEMA ANAPENDA MAISHA YA LIGI KUU YA ...LAKINI PIA AELEZEA JINSI ALIVYOCHUKIA BAADA YA KUFUNDISHWA NYIMBO YA JADI YA ARSENAL...taharifa kamili iko hapa...

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA OCTOBA 11,2013 SAA 08:25 USIKU
Mesut Ozil:Kiungo wa  Arsenal  na Ujerumani anfurahia maisha yake mapya jijini London
Mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani na kiungo wa Arsenal Mesut Ozil amekubali na kueleza  kuwa anapenda maisha ya Ligi kuu ya
soka nchini England.
Mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid , ambaye alijiunga na the Gunners kwa ada ya uhamisho ya £ 43million majira ya joto,kwa sasa ana wajibu wa kimataifa pamoja na wachezaji wenzake kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kufuzu kombe la  Dunia  leo ijumaa usiku  dhidi ya Jamhuri ya Ireland.
Lakini kwa sasa  vyombo vingi  vya habari vya Ujerumani vinaangalia  juu ya maisha mapya ya  Ozil  jijini London.

Alisema: "Baadhi ya watu walidhani  mimi itakuwa vigumu zaidi kuliko hivi sasa,lakini Per Mertesacker alinipa baadhi ya 'masomo ya kuishi ' na  imenisaidia, hivyo siwezi kufanya vitu visivyo faa."
"London ni mji wa kuvutia kuishi na mimi nimepapenda  mahali hapa katika nafasi ya muda mfupi"
"Wachezaji wenzangu wa Arsenal na wafanyakazi pamoja na makocha wote wako nyuma yangu,wamenipa muitikio mkubwa  wa kipi kikubwa ninacho waza kufanya.

Ozil akiwa ndani ya the Gunners moja ya vitu alivyofundwa ni pamoja na wimbo wa jadi mbele ya wachezaji wenzake , ingawa alikuwa ni mzoefu alikiri hakuweza kufurahia. 
Akasema: "kuimba kidogo ,kiukweli sikutaka kufanya hivyo kwa sababu sauti yangu tu haiko juu kufanya hivyo"
Alipoulizwa nini alichokuwa akiimba, alijibu: "ulikuwa ni wimbo  wa Kituruki, kwa kuwa waaminifu, Bila shaka, watu hawakuelewa nini nilikuwa naimba." 
 
 

Post a Comment

0 Comments