Ticker

6/recent/ticker-posts

ALICHOKISEMA RONALDO KUHUSIANA NA NEYMAR, KIKO HAPA...

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA OCTOBA 11,2013 SAA 07:21 USIKU

Kijana wa Brazil Neymar ameongezeka kiwango  tangu alipoondoka katika klabu ya  Santos na  kwenda  Barcelona mnamo
mwezi  Juni na anaweza kwenda juu zaidi ya hapo  na kuwa mchezaji bora duniani, kwa mujibu wa Ronaldo Luís Nazário de Lima.
"Yeye ana nifuata mimi  na nina uhakika atakuwa na kunizidi hata zaidi,"alisema mchezaji huyo wa  zamani wa Brazil na Barcelona Ronaldo akiwaambia waandishi wa habari mjini Rio de Janeiro Alhamisi.
"Kama yeye ataendelea kuwa na ubora kama huu, atakuwa mchezaji bora duniani." 
Ronaldo alisema Neymar inaweza kurusha timu yake  kwenye vizingiti  vyote,wakati  ataporudi nyumbani katika nchi yake kwa ajili ya Kombe la Dunia 2014. 
"Pamoja na kuwa kijana mdogo anayekosolewa,ameonyesha kiwango kizuri katika miezi yake michache ya kwanza nchini Hispania  na kwamba anaweza kun'gara  sambamba na wachezaji bora  duniani kama mchezaji mwenzake wa  Barca Lionel Messi na mshambuliaji wa  Real Madrid na Ureno Cristiano Ronaldo"

Ronaldo, ambaye ana kampuni yake inayoshughulikia maswala ya  masoko katika  michezo,na pia yuko katika kamati ya maanalizi ya Kombe la Dunia, lakini kwa  sasa anatumia ya zaidi ya muda wake jijini London ambapo anasomea maswala ya  biashara na masoko.

Post a Comment

0 Comments