Ticker

6/recent/ticker-posts

BARCELONA:JORDI ALBA ATAKUWA NJE WIKI SITA

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA OCTOBA 11,2013 SAA 09:35 ALFAJIRI
Beki wa kushoto wa Barcelona Jordi Alba atakuwa nje kwa  wiki
sita baada ya  kuumia mguu.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa   Hispania mwenye umri wa miaka 24 atakuwa katika wakati mgumu kwani inasemekana atakuwa  nje kwa karibu mwezi mmoja hivi.
Barca ambayo iko juu katika msimamo wa ligi kuu  baada kushinda michezo yote nane,lakini wako sawa  na  Atletico Madrid ila  tofauti kwa mabao.
Kocha Gerardo Martino atawatumia Javier Mascherano, 29, na Carlos Puyol, 35,baada ya kurudi kutoka majeruhi.
Mascherano  aliumia mguu katika mechi waliyoshinda 4-1 dhidi ya Real Sociedad, wakati nahodha wa klabu Puyol amekuwa nje tangu March baada ya kufanyiwa operesheni kubwa ya goti .
Marc Bartra, 22, imekuwa akicheza mara kwa mara katika wiki za karibuni.
Lakini ulinzi wa wacatalan hao  kuna uwezekano wa kuwa bora zaidi wakati watakapopambana na  Osasuna - baada ya mapumziko ya kimataifa, na mechi hiyo itapingwa Jumamosi ya  Oktoba 19. 

Post a Comment

0 Comments