Na.Herman Kihwili,IMEWEKWA OCTO 3,2013 SAA 08:50 USIKU
![]() |
|
Richard M.
kayombo ni mkurugenzi wa huduma na elimu wa mamlaka ya mapato Tanzania(kushoto)
|
Wito
umetolewa kwa wafanyabiashara wote nchini kununua mashine za risiti za kielektroniki ,kwani ifikapo Novemba 15
mwaka
huu,hakutaruhusiwa kufanya biashara pasipokuwa na mashine hizo.
Hayo
yamesemwa na naibu kamishna idara ya kodi za ndani Bi.Genorose Bateyuga,na
kuwataka wananchi kujua umuhimu wa kudai risiti na iwapo hawatapewa risiti
wanatakiwa kutoa taharifa katika ofisi za mamlaka ya mapato nchini.
![]() |
| Naibu kamishna idara ya kodi za ndani Bi.Genorose Bateyuga,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) |
Aidha
Genorose Bateyuga ameongeza kuwa mashine hizo zanatakiwa kutumiwa na
wafanyabiashara wote wenye kuingiza zaidi ya shilingi 45,000 kwa siku,na iwapo
mfanya biashara atakiuka agizo hilo,atapigwa faini ya shilingi milioni 3 na
iwapo akiwa amepigwa faini lakini bado ataendelea kukiuka agizo hilo,mamlaka
itachukua hatua ya kumfungia na kutangazwa kuwa uma kuwa anafanya biashara
kinyume na utaratibu.
Pia Bi.
Bateyuga amewataka wafanyabiashara kufika katika ofisi zao zilizozagaa kote
nchini kununua mashine hizo za kielektroniki ,na kuwaomba kuhakikisha wanaelekezwa jinsi ya kutumia
mashine hizo,na kusisitiza iwapo mashine hizo zitaharibika,unatakiwa kurudisha
ndani ya masaa 24 na mfanya biashara utapewa kibali maalumu cha kutumia risiti
za kawaida kwa muda.
Mshine za kielektroniki
ni muhimu kwa sababu zinamsaidia mteja kulipa kodi kilingana na unachokilipia.
Mamlaka ya
mapato nchini Tanzania(TRA) imejipanga kikamilifu kwani tangu siku ya jumatatu
ya tarehe 3 Septemba mwaka huu wafanyakazi wake wametawanyika katika sehemu
mbalimbali za kupakia mizigo kama Ubungo,Temeke,Jangwani na Kisutu.


0 Comments