Ticker

6/recent/ticker-posts

BARCELONA:MESSI AMERUDI TENA

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA OCTOBA 15,2013 SAA 09:02 ALFAJIRI

Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi amerejea kujiunga na wachezaji wenzake katika  mafunzo  jana siku ya Jumatatu baada
ya kuendelea kupata ahueni  kutokana maumivu ya paja aliyoyapata katika  mechi ya La Liga  dhidi ya  Almeria mwishoni mwa mwezi uliopita.
Mchezaji huyo wa ghali Duniani hakuweza kujiunga na Argentina, ambayo tayari imeshapata nafasi ya kushiriki katika fainali za Kombe la Dunia mwaka ujao nchini Brazil, katika mechi za mwisho dhidi ya Peru na Uruguay, ambapo yeye alibaki Barcelona kwa matibabu.
Barca  mechi yao inayofuata  ya La Liga watafunga safari kuifuata Osasuna siku ya Jumamosi, ingawa kwa mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya AC Milan itakayopigwa Jumanne ya Oktoba 22 bado haijulikani kama kocha Gerardo Martino italeta ushindani katika mchezo huo ambao watakuwa ugenini.

"Mshambuliaji wa Barca na Argentina imechukua hatua nyingine mbele kwa kupata ahueni," walisema mabingwa hao wa Kihispania kwenye tovuti yao ya (www.fcbarcelona.es) Jumatatu. 

Messi amefunga mabao nane katika mechi sita za La Liga msimu huu,na kufunga  hat-trick dhidi ya Ajax Amsterdam katika Ligi ya Mabingwa pekee. 

Post a Comment

0 Comments