Ticker

6/recent/ticker-posts

RAISI WA REAL MADRID FRORENTINO PEREZ AMESEMA BALE ANAWEZA KUCHEZA KATIKA MECHI DHIDI YA MALAGA,LAKINI KOCHA WA WALES ANASEMA MCHEZAJI HUYO ANAHITAJI MUDA ILI KUWA VIZURI

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA OCTOBA 15,2013 SAA 12:02 JIONI
Rais wa timu ya Real Madrid Florentino Perez  amesisitiza tena kuwa hakuna mashaka makubwa juu ya hali ya Gareth Bale na
anaweza kuonekana uwanjani  mwishoni mwa wiki hii.
Ripoti iliojitokeza mwishoni mwa wiki kutoka makao makuu ya Madrid lakini kwa mijibu wa gazeti la Marca ,inadai kwamba Bale alikuwa na maumivu  katika mgongo wake na anaweza kuhitaji upasuaji.
Ilidaiwa kwamba mara ya kwanza kabisa wamegundua kuhusu tatizo hilo wakati Bale akifanyiwa vipimo wakati alipojiunga na timu ya Hispania katika uhamisho ambao ulivunja rekodi ya dunia  mwanzo wa Septemba. 
Lakini Perez alipuuzia madai hayo, na alikiambia kipindi cha televisheni  Punto Pelota: "Nimeshangazwa Ni vigumu kuelewa juu ya taarifa hizi za kikatili."
"Ni mara ya kwanza mimi kusikia juu ya taarifa hizo,na gazeti  pia liliandika kwamba mimi nimeambiwa kuhusu tatizo hili wakati wa vipimo. Ni uongo kabisa."
"Mchezaji na timu yake wote tunawasiwasi kwa sababu tunamikataba na taarifa hii inaweza kuathiri, Wameweza kuisema ana ngiri wakati yeye hana na wanasheria wetu wanaangalia nini kifanyike." 
Perez amesisitiza Bale anaweza kuwepo katika mchezo dhidi ya Malaga na alisema: "Gareth yuko shwari tayari na kuna matumaini ya kucheza Jumamosi".
"Yuko katika mafunzo vizuri na anataka kucheza na kuonyesha kwamba yote hii ilikuwa  mwanzo mbaya na bahati mbaya." 

Lakini katika hatua nyingine,meneja wa Wales  Chris Coleman amesema  Gareth Bale anahitaji  kuchukua muda wa kukaa ili kuonyesha ubora wake katika timu ya Real Madrid.
Coleman ambaye hakumchezesha mchezaji huyo katika mechi ya kufuzu kombe la dunia dhidi ya Macedonia, amesema "Nashashangazwa sana labda mpaka baada ya Krismasi ,tunaweza kumuona Gareth Bare akawa vizuri tena," alisema Coleman.
 Coleman aliongeza: "Katika kambi ya mwisho hapa, nilikuwa na mengi ya kukosoa kwa kutocheza Bale, lakini mtu huyo, hakuwa katika mafunzo kabla ya msimu.
Kama huna mazoezi ya kabla ya msimu na wanatarajia kuanza na kumaliza katika mchezo,lazima kutakuwa na kasoro itakayojitokeza."
"inaweza kuchukua muda kabla ya Gareth Bare kuonekana katika ubora wake, hasa ukizingatiaziada na mazingira mapya ambayo yuko sasa." 

Post a Comment

0 Comments