Ticker

6/recent/ticker-posts

AC MILAN NA BARCELONA HAKUNA MBABE,NAYMAR NA ROBINHO WAONESHANA UPENDO WA KWELI,KWENGINEKO MASHABIKI WA NAPOLI WAANZISHA BONGE LA MTITI KATIKA MJI WA UFARANSA

 IMEWEKWA OKTOBA 23,2013 SAA 11:09 ALFAJIRI
Clash: polisi wa kutuliza ghasia wakipuliza maji ya dawa kwa mashabiki wa Napoli  barabarani kabla ya mchezo
Mashabiki wa Napoli walikuwa katika uangalizi baada ya kukimbia ghasia kaskazini mwa London wakati wao wanakabiliwa Arsenal,
lakini hapo jana pia kulikuwa na mapigano kati ya mashabiki na polisi wa Ufaransa na kufanya kuwe na ghasia kabla ya mechi hii.
Katika nafasi: polisi walikuwepo ndani ya uwanja kwa ajili ya mechi
Machoni kama watu:Mshabiki wa Napoli  Wakifurahi ndani ya uwanja, kabla ya mpira kuanza ilikuwa ni mateke
Kipigo:Shabiki Mmoja wa Napoli  mbaroni kabla ya mchezo na Marseille
Msuguano: Baadhi ya wafuasi wa Napoli wakionekana wamebeba fimbo wakikabiliana na polisi
Lakini Katika mchezo wa jana timu ya Napoli inayoongozwa na kocha Rafa Benitez,imefanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 2 kwa 1 dhidi ya Marseille katika mchezo uliopingwa nchini  Ufaransa katika uwanja wa  Stade Vlodrome.
Duvan Esteban Zapata akifunga bao la ushindi kwa Napoli
Jose Callejon (katikati) akisherehekea baada ya kufunga bao la kwanza kwa Napoli
Mabao ya Napoli yaliwekwa nyavuni na Jose Maria Callejon katika dakika ya 42 baada ya kumtoka beki na kipa wa Marseille, na bao la pili lilifungwa katika dakika ya 67 na  Duvan Zapata aliyechukua nafasi ya Gonzalo Higuain dakika ya 58 .Na bao la kufutia machozi kwa upande wa Olympique de Marseille lilifungwa na André Ayew katika dakika ya 89.
Katika mchezo mwingine Neymar na Robinho walionekana kuwa na hamu sana ya  kubadilishana mashati wakati wa mpambano wa AC Milan dhidi ya Barcelona katika Ligi ya Mabingwa  usiku wa Jumanne ... na walifanya hivyo mapema baada ya kipindi cha kwanza kuisha!
Bado mapema: Mchezaji wa AC Milan ya Robinho na Neymar wa Barcelona walibadilishana mashati kabla ya mchezo  wa AC Milan v Barcelona kuisha
 Neymar alipost picha ya shujaa wake mwenyewe  Robinho kwenye Instagram Jumanne
Robinho akiongea na Neymar baada ya filimbi ya mwisho na baada ya sare ya AC Milan 1-1 na Barcelona
Pamoja na kuwa timu moja ya taifa, Robinho bado ni mmoja wa mashujaa wakubwa wa Neymar na ndio maana wakabadlishana mashati mapema baada ya mwamuzi kupuliza kipenga kuashilia ni mapumziko.
Robinho akiwachanganya walinzi wa Barcelona na kuweza kufunga wao la kwanza kwa Milan
Mfungaji: Robinho akishangilia bao la kuongoza wakati wa mechi ya Kundi H Milan dhidi ya Barcelona
Lakini katika mchezo timu hizo mbili za AC Milan na Barcelona zimechoshana nguvu kwa kutoka sare ya 1 kwa 1, na wenyeji AC Milan ndio waliotangulia kupata bao kupitia kwa Robinho mapema katika dakika ya 9.
Na bao la Barcelona lilifungwa na Lionel Messi katika dakika ya 23.
Lionel Messi akitikisa nyavu za Milan na kusawazisha kwa upande wa Barcelona
Wachezaji wa Milan, ikiwa ni pamoja na Mario Balotelli na Sulley Muntari, wakiruka wakati Messi akipiga free-kick isiyokuwa na faida.





Post a Comment

0 Comments