Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA SEPT. 13,2013 SAA 11:45 jioni
Yanga
imepewa siku 14 kuanzia leo (Septemba 13 mwaka huu) kuwalipa waliokuwa
wachezaji wake msimu uliopita, nahodha Shadrack Nsajigwa na Stephen
Mwasika wanaoidai
klabu hiyo jumla ya sh. milioni 15.5.
Uamuzi
huo umefanywa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Septemba 12 mwaka
huu) ambapo pamoja na mambo mengine ilisikiliza madai ya wachezaji hao.
Fedha
hizo ni ada ya usajili ambayo klabu hiyo ilikubaliana na wachezaji hao
wakati ikiwasainisha mikataba. Yanga imeshawalipa sehemu ya fedha
walizokubaliana na kiasi hicho ndicho bado hakijalipwa. Nsajigwa anadai
sh. milioni 9 wakati Mwasika ni sh. milioni 6.5.
SIMBA UWANJA WA TAIFA, YANGA IKO MBEYA VPL
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia raundi ya tatu kesho (Septemba 14 mwaka
huu) kwa timu zote 14 kushuka viwanjani huku masikio ya washabiki wengi
yakielekezwa kwenye mechi kati ya Simba na Mtibwa Sugar na ile kati ya
Mbeya City na Yanga.
Simba
inaikaribisha Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika
mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana kutoka Dodoma.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 viti vya bluu na kijani,
sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C na B wakati VIP A
itakuwa sh. 20,000.
Pia
Azam TV itautumia mchezo huo kwa ajili ya mazoezi (broadcast training)
kwa wafanyakazi wake. Hivyo mechi hiyo haitarekodiwa au kuoneshwa moja
kwa moja.
Katika
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, shughuli itakuwa kati ya
mabingwa watetezi Yanga na wenyeji wao Mbeya City SC. Mwamuzi Andrew
Shamba kutoka Pwani ndiye atakayepuliza filimbi wakati Kamishna wa mechi
hiyo James Mhagama kutoka Songea.
Mechi
nyingine za ligi hiyo ni Coastal Union na Tanzania Prisons (Uwanja wa
Mkwakwani, Tanga), Ruvu Shooting na Mgambo Shooting (Uwanja wa Mabatini
mkoani Pwani), Oljoro JKT na Rhino Rangers (Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha), Kagera Sugar na Azam (Uwanja wa
Kaitba, Bukoba), na Ashanti United na JKT Ruvu (Uwanja wa Azam Complex,
Dar es Salaam).

0 Comments