Ticker

6/recent/ticker-posts

30 WAITWA KAMBINI TWIGA STARS

 Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA SEPT. 13,2013 SAA 11:49 jioni

Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage ameita kambini kikosi cha wachezaji 30, wengi wao wakiwa vijana ikiwa ni mwendelezo wa programu ya kujenga timu hiyo.
Kambi hiyo itakuwa jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 15 hadi 26 mwaka huu. Vijana wengi wamejumuishwa ikiwa
ni hatua ya mwanzo ya kuandaa timu itakayocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20.

Kaijage amesema pamoja na malengo hayo kwa timu ya vijana, bado maana kubwa inabaki kuandaa Twiga Stars iliyo imara kwa ajili ya mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Amesema Twiga Stars haikabiliwi na mashindano yoyote mwaka huu, hivyo lengo ni kuijenga upya ndiyo maana haichezi michezo ya kimataifa ya kirafiki hadi itakapofika wakati wake.

Utaratibu huo ulianza kuanzia kambi ya Machi mwaka huu, na ndio umezaa timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ambayo sasa itashiriki mashindano ya Kombe la Dunia.

Wachezaji walioitwa ni Amina Ally (Lord Barden, Pwani), Asha Rashid (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Belina Julius (Lord Barden, Pwani), Donisia Daniel (Lord Barden, Pwani), Esther Chabruma (Sayari Queens, Dar es Salaam), Eto Mlenzi (JKT, Dar es Salaam) na Evelyn Sekikubo (Mburahati Queens, Dar es Salaam).

Fatuma Bushiri (Simba Queens, Dar es Salaam), Fatuma Hassan (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Fatuma Issa (Evergreen, Dar es Salaam), Fatuma Mustafa (Sayari Queens, Dar es Salaam), Fatuma Omari (Sayari Queens, Dar es Salaam), Flora Kayanda (Tanzanite, Dar es Salaam) na Gerwa Lugomba (Umisseta, Kanda ya Ziwa).

Hamisa Athuman (Marsh Academy, Mwanza), Maimuna Hamisi (Airtel Rising Star, Ilala), Maimuna Said (JKT, Dar es Salaam), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Mwapewa Mtumwa (Sayari Queens, Dar es Salaam), Pulkeria Charaji (Sayari Queens, Dar es Salaam) na Rehema Abdul (Lord Barden, Pwani).

Sabahi Hashim (Umisseta, Zanzibar), Semeni Abeid (Tanzanite, Dar es Salaam), Sharida Boniface (Makongo Sekondari, Dar es Salaam), Sofia Mwasikili (Sayari Queens, Dar es Salaam), Tatu Idd (Lord Barden, Pwani), Therese Yona (TSC Academy, Mwanza), Vumilia Maarifa (Evergreen, Dar es Salaam), Yulitha Kimbuya (Marsh Academy, Mwanza) na Zena Khamis (Mburahati Queens, Dar es Salaam).   


MJINI MAGHARIBI KUCHEZA FAINALI COPA
Mjini Magharibi imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya kuing’oa Temeke kwenye nusu fainali iliyochezwa leo (Septemba 13 mwaka huu) asubuhi Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam.

Ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa dakika za 30 na 63 kupitia Juma Ali Yusuf ndiyo yaliyoipa Mjini Magharibi tiketi ya kucheza fainali itakayofanyika kesho (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 9 alasiri.

Mjini Magharibi itacheza fainali hiyo na mshindi wa nusu fainali ya pili inachezwa leo jioni kwenye uwanja huo huo kati ya mabingwa watetezi Morogoro na Ilala.

Kwa upande wa wasichana Ilala imetinga fainali baada ya kuifunga Kinondoni mabao 2-0 katika nusu fainali ya kwanza. Mabao ya washindi yalifungwa dakika ya 27 na Fatuma Bahau wakati Happiness Lazoni alifunga la pili dakika ya 39.

Nusu fainali ya pili kwa wasichana itakuwa kati ya Mwanza na Mbeya.

Post a Comment

0 Comments