Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 13,2013 SAA 4:19 USIKU
Brendan
Rodgers amesema Daniel Sturridge anaweza kuwa vizuri
katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Swansea City siku ya
Jumatatu licha ya mshambuliaji huyo kukosa michezo miwili ya kufuzu kombe la Dunia na timu yake ya taifa la England kwa sababu ya kuumia.
Sturridge , ambaye amefunga mabao matano kwa Liverpool , ikiwa ni
pamoja na kushindi katika michezo yote mitatu ligi kuu,na na Rodgers anamatumaini atarudi kuendelea kusaidia timu hiyo.
Baada ya kupata majeraha katika mguu na kumzuia kucheza katika michezo ya nchi yake dhidi
ya Moldova na Ukraine na kusababisha maneno maneno katika magazeti, lakini Rodgers alisema
dhamira ya Sturridge nchini Uingereza haipaswi kuhoji.
"walikuwa ni wataalam wa tiba ambao walifanya uamuzi - na si Daniel Sturridge,Amerudi,kwani kulikuwa na maboresho kidogo," Rodgers aliwaambia waandishi wa habari.
Liverpool wanaoendesha wimbi la matumaini, hasa baada ya kummchapa Manchester
United kabla ya mapumziko ya kimataifa, na kikosi cha Rodgers kimeonekana
kuimarika baada ya kupatikana kwa nyuso tatu mpya ambazo zinatarajiwa kuwepo katika mchezo dhidi ya Swansea.
Walinzi Tiago Ilori na Mamadou Sakho walikuwa wamesaini siku ya tarehe ya
mwisho ya dirisha la usajili kufungwa kama ilivyokuwa mchezaji wa Chelsea Victor Muses aliyechukuliwa kwa mkopo wa muda mrefu na wote wanaweza kuwa sehemu ya wachezaji watakao cheza siku ya Jumatatu.

0 Comments