Ticker

6/recent/ticker-posts

DAVID MOYES AJITETEA KWA KUTOMTUMIA SHINJI KAGAWA

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 14,2013 SAA 10:36 USIKU

David Moyes amesema sababu kuu ya kwa nini baadhi ya wachezaji wamekuwa na majukumu mdogo hadi sasa msimu huu ni
kwamba masharti ya  kimataifa yamekuwa magumu.
Kiungo wa Kijapani  Shinji Kagawa ambaye alicheza kwa  dakika saba wakati Moyes akiwa katika timu hiyo,akitokea katika  benchi  katika mechi ya Community Shield  ambapo walishinda dhidi ya Wigan  mwezi Agosti na alikiri mapema wiki hii kwamba alikuwa amechanganyikiwa, baada ya kusema: ."Tafadhali muulize David Moyes kwa nini mimi sio pendekezo lake?" 
Bosi huyo wa United alifafanua kwa maelezo rahisi, ambayo yanatokana na  kuchelewa kurudi kwa Kagawa  kabla ya msimu na kufuatia Kombe la Shirikisho na ni pamoja na safari mbili za kurudu katika nchi za  Mashariki ya Mbali tangu  na kutimiza wajibu  kitaifa. 
Shinji Kagawa:Achezi mara kwa mara kutokana masharti ya kimataifa

"Kuna wachezaji wengi ambao hawana umuhimu bado," alisema.
"Lakini kama utakuwa  unaona miongoni mwao walikuwa wamechelewa kurudi kutokana na kuwa na wajibu wa kimataifa, baada ya Kombe la Shirikisho,kwaiyo walikuwa mbali kwa ajili ya michezo ya kirafiki ya kimataifa, na muda hukimbia,walikuwa mbali tena kwa ajili ya michezo mingine ya  kimataifa"
Kama ukiangalia sababu kwa nini watu hawachezi,huwezi kufanya kitu zaidi kama wao wanapotakiwa hawatokei"

Mwisho wa yote David Moyes akamalizia kwamba "Kama wewe unacheza katika klabu ya  Manchester United daima ujue kuwa kuna mtu huko nje yuko tayari kuchukua jezi yako,kwa maana hiyo ni ni juu yako na kupambana na  kuhakikisha kuitunza." 

Post a Comment

0 Comments