Ticker

6/recent/ticker-posts

VILLARREAL 2 REAL MADRID 2:BALE AHALALISHA UHAMISHO WAKE WA REKODI DUNIA KWA KUPACHIKA KIMOJA,LAKINI RONALDO AMUHAKIKISHIA KUWA BADO YUMO

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 15,2013 SAA 8:08 USIKU
Bale wa Madrid : Winga wa zamani wa Tottenham  Gareth Bale anafurahia mechi yake ya kwanza na goli lake la kwanza kwa kuonyesha alama yake ya  biashara
Ni goli la 203 katika michezo 203 kwa Cristiano Ronaldo; na goli la kwanza katika mchezo wa kwanza kwa Gareth Bale,na hiyo ilikuwa
katika mchezo wa usiku wa kuamkia  leo uliomalizika kwa sare ya mabao 2 kwa 2 kati ya Villarreal na Real Madrid.
Mwanzo mzuri:Kuanza kubwa: Bale akisheherekea kwa pamoja na  Daniel Carvajal
Haikuwa raisi kwa Real Madri lakini Gareth bale alipata bao lake la kwanza dakika ya 38 katika timu hiyo,bao lililokuwa ni la kusawazisha kwa timu ya Real Madrid kwani tayari Villarreal walikuwa wameshapata bao la kuongoza kupitia kwa mchezaji wao Ruben Cani katika dakika ya 21.
Villarreal walifunga bao la ufunguzi kupitia kwa Cani dakika ya 21
Furaha: Bale alikuwa ni furaha kupitiliza alivyo funga goli,na kumfanya kocha Carlo Ancelotti kunyanyuka katika kiti.


Wameanza kucheza kwa pamoja:: Bale na Cristiano Ronaldo wamepangwa kwa mara ya kwanza kuanza kuchzea katika timu hiyo
Watu Muhimu: wachezaji watatu ambao wanategemewa kwa sasa ndani ya Madrid,Isco(kushoto), Ronaldo na Bale
Katika kipindi cha pili  katika dakika ya 60  kilifanyika mabadiliko kwa timu ya Real Madridi kwa kumtoa Gareth Bale na kumuingiza Di Maria,ndipo kukamuongezea kasi Cristiano Ronaldo na kuweza kuipatia Real Madrid bao lao la pili katika dakika ya 64.
Kwani nini, Gareth?: Cristiano Ronaldo akishangilia  baada ya kuwapatia Madrid bao la pili  kuongoza, muda mfupi baada ya Bale  kubadilishwa
 Lakini lakini wahenga wanasema nyumbani ni nyumbani,kwani kwa nguvu ya mashabiki na hali ya kasi ya mchezo walioionyesha vijana wa Villarreal,wakaweza kuchomoa kupitia kwa mchezaji wa zamani wa Barcelona na Tottenham Hotspur kabla hajaamia Mallorca na kuchukuliwa na Villarreal kwa uhamisho uliofanyika July  9, 2013,hapo  Jamii na Michezo inamzungumzia Giovani dos Santos Ramírez,aliyepachika bao zuri katika dakika ya 70,na mpaka ngoma inamalizika mabao ni mawili kwa mawili.

Mchezaji  wa zamani wa Spurs : Giovani Dos Santos (katikati) waliwai kucheza pamoja na Bale wakiwa Tottenham
Ngumu kuamini: Bale na wenzake wakiangalia wakati wachezaji wa  Villarreal wakishangilia
Mgumu: kocha bora  wa Real Madrid Carlo Ancelotti , na wachezaji wake wengi wapya
Maagizo: Pamoja na kikwazo cha lugha, Bale alijaribu kuelekeza wenzake
Kikosi cha Real Madrid: Diego Lopez, Carvajal, Pepe, Ramos, Nacho, Illarramendi (Khedira 60), Modric, Bale (Di Maria 60), Isco, Ronaldo, Benzema (Morata 72)
Akiba wasiotumika : Casillas, Casemiro, Jesé, Llorente
wafungaji: Bale, Ronaldo
kikosi cha Villareal: Asenjo, Mario, Musacchio, Dorado, Costa, Aquino, Trigueros, Bruno, Cani, Giovani, Pereira (Uche 64).
Akiba wasiotumika: Carlos, Perez, Pina, Iniguez, Perbet, Gabriel.
wafungaji: Cani, Giovani






Post a Comment

0 Comments