Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 19,2013 SAA 8:00 USIKU
Lionel
Messi amefanikiwa kupiga hat-trick katika ushindi wa bao 4 kwa 0 kati ya timu yake ya Barcelona na timu ya Ajax mchezo
uliokuwa wa Kundi H katika ligi ya mabingwa balani ulaya uliopigwa katika Uwanja wa Nou Camp.![]() |
| Usahihi: Messi bao lake la kwanza lilipatikana kwa free-kick katika dakika ya 22 |
Mshambuliaji huyo
wa Argentina alikuwa na wasaa mzuri baada ya kupiga bao lake la kwanza kwa mkwaju wa free-kick ndani ya dakika ya 22 na kisha kuzalisha bao mbili katika dakika ya 55 na 75 lakini bao la tatu la timu ya Barcelona,alifunga Gerard Pique kwa msaada wa messi katika dakika ya 69 kabla ya kupisha na nafasi yake kuchukuliwa na Bartra katika dakika ya 80.
![]() |
| Ruka juu: Pique aliiwezesha Barcelona kwa kuipatia bao la tatu |
Messi,
labda alitetemeshwa na Cristiano Ronaldo katika mchezo wa Real Madrid
usiku wa Jumanne,na sasa ana mabao 62 katika michezo ya Ligi ya Mabingwa na kuwa na rekodi ya kupiga hat-tricks 4.
![]() |
| Kuchanganyikiwa: Neymar alikasirika baada ya kukosa bao,kabla ya kutolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Pedro dakika ya 72 |
Kwa upande wa timu ya ajax kwa kweli walikuwa hawana bahati katika mchezo wa jana,maana walipoteza penalti iliyopigwa na Kolbeinn Sigthorsson katika dakika ya 77 na kisha penalti hiyo kupanguliwa na kipa Victor Valdes.
Akiba wasotumika : Pinto, Montoya, Song, Tello.
Wafungaji: Messi (22, 55 & 75), Pique (69)
Kiakosi cha Ajax: Vermeer, van Rhijn, Denswil, Moisander (van der Hoorn 73), Blind (Schone 78), Poulsen, de Jong (Serero 59), Duarte, Bojan, Sigthorsson, Boilesen.
Akiba wasiotumika : Cillessen, Fischer, Sana, Hoesen.
BOFYA HAPA KWA MATOKEO KAMILI,RATIBA NA MSIMAMO WA LIGI YA MABINGWA BALANI ULAYA




0 Comments