Ticker

6/recent/ticker-posts

LIGI KUU ENGLAND:KIUNGO PHILIPPE COUTINHO KUWA NJE MPAKA MWISHONI MWA MWEZI OKTOBA

  Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 18,2013 SAA 3:0 USIKU

Liverpool wamethibitisha Philippe Coutinho Atakuwa  nje mpaka mwishoni mwa mwezi Oktoba baada ya kuumia bega lake katika mchezo uliomalizika kwa sare ya 2-2 dhidi ya
Swansea uliopigwa siku ya Jumatatu usiku.
Mbrazil ambaye alibadilishwa na nafasi yake kuchukuliwa na  Iago Aspas dakika 55 kwenye Uwanja wa Liberty baada ya kuanguka kufuatia changamoto kutoka kwa  nahodha  wa Swansea  Ashley Williams.
Mchezaji huyo mwenye Miaka 21-aliondoka uwanja huku mkono wake ukiwa umeshikilia bega  na baada ya mchezo  meneja wa Liverpool Brendan Rodgers aliaelezea taharifa kuhusiana na Coutinho "alikuwa amejeruhiwa  sana tulipomuangalia katika chumba kubadilisha." 
Siku ya Jumatatu, Rodgers alisema anatumaini  kuumia  kwa Coutinho kulikuwa ni zaidi ya kuvilia damu lakini sasa ni wazi kwamba kuumia kwake kulikuwa na  mbaya zaidi kuliko awali walivyofikili. 
Sasa mchezaji huyo anajiunga na wenzake Glen Johnson, Aly Cissokho na Sebastian Coates ambao wote wako nje kwa majeraha  katika kikosi cha  Liverpool, wakati Daniel Sturridge akirejea kikamilifu baada ya kuwa nje kwa majeraha,na kama unakumbuka alipiga bao moja katika mchezo wa siku ya jumatatu dhidi ya Swansea City.

Post a Comment

0 Comments