Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 10,2013 SAA 3:12 USIKU
Kampuni ya Disney imeleta maendeleo baada ya kugundua kifaa cha kusambaza sauti kwa njia ya mwili wa binadamu.
Teknolojia hiyo inayojulikana kama Ishin-Den-Shin inatumia kipaza sauti kurekodi sauti na baada ya hapo huibadilisha kuwa
katika hali isiyosikika na kuisambaza kwa njia ya mwili
wa mtu aliyeshika kipaza sauti.
Ikiwa umegusa sehemu ya ndani ya sikio la mtu, sauti ya msemaji hai inaundwa na ujumbe hufika kwa mtu mwingine kama mnanong'onezana.
Sauti inaweza kupitishwa kutoka mtu kwa mtu na kutumia mawasiliano yeyote ya kimwili.
Teknolojia,
ambayo ilitengenezwa katika katika kampuni ya utafiti ya Disney Utafiti mjiwa Pittsburgh nchini marekani, ilipokea
heshima wiki hii baada ya kuorodheshwa katika tamasha la Ars Electronica mjini Linz,
Austria.
VIDEO IKO HAPO CHINI

0 Comments