Na.Boniface Wambura pamoja na Herman kihihwili,IMEWEKWA AGOSTI 29,2013 SAA 10:40 jioni
Mechi
ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Coastal Union iliyochezwa
jana (Agosti 28 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
imeingiza sh. 152,296,000.
Watazamaji 26,137 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 14 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1.
Viingilio
katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh.
15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 36,947,427.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 23,231,593.22.
15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 36,947,427.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 23,231,593.22.
Mgawo
mwingine ni asilimia 15 ya uwanja sh. 18,786,827.52, tiketi sh.
3,818,890, gharama za mechi sh. 11,272,096.51, Kamati ya Ligi sh.
11,272,096.51, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
5,636,048.26 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
sh. 4,383,593.09.
Katika hatua nyingine Michuano
ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15
inayoshirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani inaanza kutimua
vumbi Septemba 2 mwaka huu katika vituo sita tofauti.
Kwa
mujibu wa ratiba iliyopangwa leo (Agosti 29 mwaka huu), kituo cha
Mwanza mechi zake zitachezwa katika viwanja vya Alliance ambapo timu
zitakazofungua dimba ni Kagera vs Kigoma, Mara vs Tabora, Simiyu vs
Geita na Mwanza vs Shinyanga.
Kituo
cha Mbeya ambapo mechi zitachezwa viwanja vya Iyunga ni Katavi vs
Njombe, na Ruvuma vs Mbeya. Kituo cha Pwani ni Ilala vs Kaskazini
Unguja, na Lindi vs Pwani.
Ufunguzi
katika kituo cha Arusha ambapo mechi zake zitachezwa Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta AMri Abeid ni Manyara vs Kilimanjaro, na
Arusha vs Singida.
Uwanja
wa Jamhuri ambapo utatumika kwa mechi za kituo cha Morogoro, Tanga
itacheza na Dodoma wakati Morogoro itaumana na Temeke. Mjini Zanibar
kwenye Uwanja wa Chuo cha Amaan ni kati ya Kaskazini Pemba na Mjini
Magharibi, na Kusini Pemba dhidi ya Kusini Unguja.
Picha na blog ya Coastal union
0 Comments